Advertisements

Thursday, December 28, 2017

WAZIRI LUKUVI ATOA ONYO KWA VISHOKA WA ARDHI

Serikali imekemea baadhi ya wawekezaji wanaotumia vibaya jina la Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuwatoa wananchi katika maeneo yao kwa kisingizio cha kupewa kibali na wizara hiyo wakati sio kweli.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri mwenye dhamana ya Wizara ya Ardhi William Lukuvi ambapo amewaonya baadhi ya wawekezaji ambao wameonekana kushirikiana na baadhi ya watumishi wa serikali katika kunyang'anya haki za wananchi kitendo ambacho amesema kwa utawala wa serikali hii ya awamu ya tano hakina nafasi.

Ameongeza kwamba, kwa sasa serikali inaendelea na zoezi la kurudisha ardhi ya wananchi mikononi mwao bila ya gharama yeyote na kwa yale maeneo ambayo yatabainika kuwa na ukiukwaji wa umiliki watayarudisha kwa wenyewe ili kuendelezwa.

Mh. Lukuvi amesema zoezi la utambuzi wa umiliki wa maeneo na urasimishaji ni endelevu kwa mikoa yote nchini lengo ni kujua maeneo yanayomilikiwa kihalali na kumaliza migogoro ya ardhi ambayo imeonekana bado ni changamoto kwa maeneo mengi mijini na vijijini.

No comments: