Advertisements

Thursday, February 15, 2018

RAIS SHEIN AHUDHURIA MAHAFALI YA 13 YA SUZA ZANZIBAR LEO

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza Dk. Ali Mohamed Shein pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) akihutubia wakati wa hafla ya Mahafali ya 13 ya Chuo hicho yaliofanyika katika ukumbi mpya wa SUZA wa Dk Ali Mohamed Shein.(Picha na Ikulu).
  BAADHI ya Wakufunzi na Wahitimu wa Mahafali ya 13 ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) (Picha na Ikulu)
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar(SUZA) Dk. Ali Mohamed Shein, akimtunuku Shahada ya Uzamivu ya Kiswahili Salma Omar Hamad, wakati wa hafla ya Mahafali ya 13 ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar ( SUZA) jumla ya wahitimu watano wametunukiwa Shadaha hiyo.
 WAHITIMU wa Shahada ya Uzamivu ya Kiswahili wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) wakati akihutubia na kutowa nasaha zake kwa wahitimu wa mahafali ya 13 ya SUZA.
 WAHITAJI wa Stashahada ya Utibabu wakila kiapo baada ya kutunukiwa stashahada katika hafla ya Mahafali ya 13 ya Chuo Kikuu cha Taifa SUZA,Tunguu yaliofanyika katika ukumbi mpya wa Dk. Ali Mohamed Shein,Tunguu Zanzibar.
 WAHITIMU wa Shahada ya Uzamili ya Sanaa ya Kiswahili wakitunukiwa shahada yao wakati wa mahafali ya 13 ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA, wakati wa mahafali hayo yaliofanyika katika ukumbi mpya wa Dk. Ali Mohamed Shein, Tunguu Zanzibar.
 BAADHI ya Waalikwa katika Mahafali ya 13 ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA ) wakiwa katika ukumbi wa mahafali hayo wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA)

No comments: