Advertisements

Sunday, April 22, 2018

KATIBU MKUU WA MAMBO YA NJE AKUTANA NA BALOZI WA CHINA NCHINI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke kuhusu Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jukwaa la Ushirikiano wa Afrika na China (FOCAC) utakaofanyika mwezi Septemba, 2018 nchini China. Mkutano huo ambao utajadili masuala mbalimbali kwa maendeleo ya Bara la Afrika utatanguliwa na vikao vya maafisa waandamizi na vile vya mawaziri. Kikao kati ya Prof. Mkenda na Balozi Wang Ke kimefanyika Wizarani tarehe 21 Aprili, 2018 
Maafisa kutoka Ubalozi wa China nchini wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Mkenda na Balozi Wang Ke (hawapo pichani) 
Prof. Mkenda akimsikiliza Balozi Wang Ke alipokuwa akimweleza kuhusu hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya Mkutano wa FOCAC utakaofanyika mwezi Septemba, 2018 nchini China 
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nao wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Mkenda na Balozi Wang Ke (hawapo pichani). Kulia ni Bi. Berha Makilagi na Bw. Halmesh Lunyumbu. 
Mkutano ukiendelea 
Picha ya pamoja

No comments: