Advertisements

Sunday, April 29, 2018

Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya waadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambayo iliambatana na maonesho ya bidhaa za viwanda vya Tanzania

Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Pindi Chana akiwakaribisha wageni waalikwa katika ufunguzi wa siku ya Tanzania ambayo huadhimishwa tarehe 26 Aprili siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Hafla ya maadhimisho hayo ilifanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Kenyatta Jijini Nairobi, Kenya. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Ababu Namwamba ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar akihutubia wageni waalikwa waliohudhuria katika mchaparo ulioandaliwa na ubalozi wa Tanzania nchini Kenya tarehe 26 April 2018. 
Viongozi wa Serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jamhuri ya Kenya na Mkuu wa Mabalozi nchini Kenya wakikata keki katika kusheherekea maadhimisho ya muungano huo. 
Viongozi wa Serikali kutoka Kenya na Tanzania wakifuatilia ufunguzi wa hafla hiyo, kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kenya, Balozi Macharia Kamau, Naibu Waziri Viwanda na Biashara, Mhe. Hassan Hafidh, Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje, Mhe. Ababu Namwamba na Balozi mteule wa Jamhuri ya Kenya nchini Tanzania, Mhe. Kazungu Kambi. 
Viongozi pamoja na wageni waalikwa wakisherehekea kwa pamoja muungano wa Tanganyika na Zanzibar. 
Sehemu ya waheshimiwa mabalozi na Wakuu wa mashirika ya kimataifa wanaowakilisha nchini Kenya wakifatilia hafla hiyo. 
Sehemu nyingine ya wawakilishi hao nchini Kenya wakifuatilia hafla. 
Sehemu ya mabalozi wa Afrika wakifuatilia hafla ya maadhimisho ya miaka 54 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar. 
Mhe. Naibu Waziri Namwamba akisalimiana na Mhe. Naibu Waziri Hafidh. 
Sehemu ya wajumbe wa kamati ya maandalizi, viongozi na wageni waalikwa wakifuatilia hafla ya maadhimisho ya Muungano. 
Picha ya pamoja 
Kikundi cha muziki wa taarabu cha Zanzibar Culture group kikitumbuiza. 
Wahudumu wakihudumia vinywaji kutoka kampuni za kitanzania.

No comments: