Kaimu Balozi wa Marekani, Dk. Inmi Patterson akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya, Dk. Faustine Ndugulile wakati alipotembelea hospitali ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam jana ambapo Serikali ya Marekani, kupitia Mpango wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), umetangaza fedha zaidi Dola Milioni 512 (takribani Shilingi Trilioni 1.17) kupambana na janga la VVU/Ukimwi nchini Tanzania. (Picha: Kwa Hisani ya Ubalozi wa Marekani).
The ChargĂ© d’Affaires of the United States Embassy, Dr. Inmi Patterson and the Deputy Minister for Health, Dr. Faustine Ndugulile address the media during at the Mnazi Mmoja Hospital in Dar es Salaam yesterday where the US government, through the President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR), announced an additional $512 million (approximately 1.17 trillion TZS) to combat the HIV/AIDS epidemic in Tanzania. (Photo: Courtesy of the US Embassy).
|
Ubalozi wa Marekani
Dar es Salaam
TANZANIA
|
Mei 4, 2018
TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
Marekani yaahidi
tena kupambana na VVU/Ukimwi nchini Tanzania
Dar es Salaam, TANZANIA. Ijumaa hii,
Mei 4, Kaimu Balozi wa Marekani nchini Dk. Inmi Patterson ametangaza wakati wa
ziara yake katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam akiwa na Naibu Waziri
wa Afya Faustine Ndugulile, kwamba Serikali ya Marekani, kupitia Mpango wa Rais
wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), umeahidi fedha zaidi Dola Milioni
512 (takribani Shilingi Trilioni 1.17) kupambana na janga la VVU/Ukimwi nchini
Tanzania. Ukiwa umeandaliwa kwa ushirikiano na serikali ya Tanzania, Mpango wa PEPFAR
nchini unalenga kudhibiti janga la VVU/Ukimwi ifikapo Septemba 2019. Serikali ya Marekani, kupitia PEPFAR, imetumia
zaidi ya Dola Bilioni 4.5(takribani Shilingi Trilioni10.26) kuzuia maambukizi
ya VVU/Ukimwi nchini toka 2004.
“Ninayo furaha kutangaza leo kwamba
kupitia PEPFAR, Serikali ya Marekani itatumia fedha zaidi Dola Milioni 512 (takribani
Shilingi Trilioni 1.17) kuboresha kinga ya VVU, upimaji na tiba nchini Tanzania
hadi Septemba 2019. Matokeo kutoka Utafiti wa Viashiria vya Ukimwi Tanzania ya
Desemba 2017 yametuonyesha kwamba Tanzania iko nyuma ya nchi nyingine za
kikanda. Mathalan, ni karibu nusu tu ya waathirika wa VVU nchini waliopimwa na
kujua kwamba wana VVU. Tanzania inabidi irudi katika mstari na hii itahitaji
juhudi kubwa katika uelimishaji umma na watu kupimwa, juhudi za haraka kuendana
na sera mpya, na utekelezaji wa haraka wa sera hizo.”
PEPFAR inahamasisha kila mtu, hususan
wanaume, kuongea na wafanyakazi wa afya kuhusu kupimwa VVU. Mtu yeyote
anayegundulika kuathirika na VVU anaweza kuanza matibabu mara moja. Takribani
Watanzania milioni moja walioathirika na VVU wako katika tiba ya kuokoa maisha,
na wengi wao wanaishi maisha marefu na ya afya na wana viwango vya chini vya
virusi kiasi kwamba hawawezi kuwaambukiza wengine, wakiwemo wenza wao na
watoto.
Kwa taarifa zaidi kuhusu PEPFAR nchini
Tanzania tafadhali tembelea tovuti ya Ubalozi wa Marekani: https://tz.usembassy.gov/our-relationship/pepfar/.
Kwa
mawasiliano zaidi kuhusu hii taarifa, tafadhali piga simu Ubalozi wa Marekani Ofisi
ya Habari Simu: +255 22 229-4000 au baruapepe: DPO@state.gov.
Usuli kuhusu
Mpango wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) nchini Tanzania
Usuli
wa mpango na takwimu za matokeo ya mpango:
• Katika
mwaka wa fedha2017 pekee, PEPFAR iliweza kupima VVU kwa Watanzania milioni 9.
• PEPFAR
inahudumia Watanzania 950,000 walio katika tiba ya kuokoa maisha yao (antiretroviral
treatment); Lengo: Watanzania milioni moja kuwa katika tiba ya kuokoa maisha
yao ifikapo mwisho wa 2018
• Katika
mwaka wa fedha 2017, PEPFAR iliweza kutoa tiba ya kuokoa maisha kwa akina mama
wajawazito 56,000 ili kuzuia maambukizi ya VVU kati ya mama na mtoto.
Tangu
PEPFAR ilipoanzishwa mwaka 2003:
• Vifo
vinavyohusiana na Ukikwi vilipungua kwa asilimia70, kutoka 110,000 mwaka 2003 hadi
33,000 mwaka 2016
• Maambukizi
mapya kwa mwaka yameshuka kwa karibu
nusu kutoka 100,000 mwaka 2003 hadi 55,000 mwaka 2016
• Mpiango
ya VVU Tanzania ilizuia maambukizi mapya milioni 1.1 na vifo 690,000
Ahadi ya PEPFAR ya
miaka 15 kwa Watanzania inaashiria thamani ya mahusiano ya muda mrefu kwa watu
wa Tanzania:
• Kupitia
PEPFAR, Serikali ya Marekani imetumia takribani Shilingi Trilioni 9 (Dola
Bilioni 4 )
• Fedha
kwa mwaka 2018 ni zaidi ya Shilingi Trilioni1 (Dola Milioni 512)
• PEPFAR
kwa sasa inatoa asilimia 73.8 ya fedha kwa ajili ya miradi ya VVU nchini
Tanzania
• PEPFAR
inatoa asilimia 68.0 ya fedha kwa ajili ya dawa za kufubaza (ARVs) na asilimia
81.3 ya fedha kwa ajili ya vipimo vya haraka.
No comments:
Post a Comment