|
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
FURSA ZA UFADHILI WA MAFUNZO KWA WATUMISHI
WA UMMA
Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea fursa za ufadhili
wa masomo ya muda mrefu katika sekta ya miundombinu chini ya program iitwayo “Global Infrasructure Development Scholarship
Program (GIDSP) kutoka Jamhuri ya Korea.
Mafunzo
haya ambayo ni kwa ajili ya Watumishi wa Umma yatafanyika katika Chuo Kikuu cha
Seoul (UOS) nchini Korea kuanzia mwezi Agosti 2018 hadi Desemba 2019.
Waombaji
wa mafunzo haya wanatakiwa kutuma maombi yao moja kwa moja kwenye Chuo Kikuu
cha Seoul (UOS). Maelezo ya ziada kuhusu mafunzo haya na namna ya kutuma maombi
yanapatikana kupitia tovuti ya http://isus.uos.ac.kr
au maombi yatumwe kwa barua pepe ifuatayo: mipd@uos.ac.kr. Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 18 Mei, 2018.
Mafunzo
haya yanaratibiwa na Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano.
Imetolewa na:
Kitengo cha
Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
03 Mei, 2018
No comments:
Post a Comment