Advertisements

Friday, June 8, 2018

KIKOSI KAZI CHA KITAIFA CHA MPANGO WA SERIKALI KUHAMIA DODOMA CHATEMBELEA ENEO LITAKALOJENGWA BWAWA LA FARKWA CHEMBA

Katibu wa Kikosi kazi cha Kitaifa cha kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akiweka sahihi katika kitabu cha wageni walipotembelea eneo la Farkwa ambapo linatarajiwa kujengwa Bwawa la kuhifadhia maji katika Kijiji cha Mombose kata Farkwa Wilaya ya Chemba Dodoma Juni 6, 2018
Mhandisi wa Maji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Annali Mwahalende akitoa maelezo kuhusu eneo la Farkwa linalotarajiwa kujengwa bwawa la kuhifadhia maji kwa Kikosi kazi cha kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma kinachoratibiwa na Idara ya Uratibu wa shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya kuratibu mpango wa Serikali kuhamia Dodoma wakiwa katika eneo la Farkwa linalotarajiwa kujengwa bwawa la kuhifadhia maji walipotembelea kukagua eneo hilo Wilayani Chema Jijini Dodoma.
Katibu wa Kikosi kazi cha Kitaifa cha Kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akipata maelezo ya eneo la Farkwa kutoka kwa Mtendaji wa Kata ya Farkwa Bw.John Wenga walipotembelea kukagua eneo hilo linalotarajiwa kujengwa bwawa la kuhifadhia maji Wilayani Chemba Mkoani Dodoma.
Katibu wa Kikosi kazi cha Kitaifa cha kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe akipata maelezo ya eneo la Farkwa kutoka kwa Mtendaji wa Kata ya Farkwa Bw.John Wenga walipotembelea kukagua eneo hilo linalotarajiwa kujengwa bwawa la kuhifadhia maji Wilayani Chemba Mkoani Dodoma
Muonekano wa Mto wa Mombose Unaotarajiwa kukusanya maji kwa ajili ya Bwawa la Farkwa litakalojengwa Wilayani Chemba Mkoani Dodoma.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU - DODOMA)

No comments: