Advertisements

Friday, July 6, 2018

MIFUGO ITAKAYOKAMATWA KWENYE MAENEO YA HIFADHI ITATAIFISHWA BILA YA HURUMA - DK. KIGWANGALLA

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Mhe. Said Mtanda (kushoto) alipowasili wilayani hapo jana kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja  ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Rukwa. Kulia ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa, Albinus Mugonya.

Na Hamza Temba, Nkasi Rukwa

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametangaza zoezi rasmi la kuanza kutaifishwa mifugo itakayokutwa kwenye maeneo ya hifadhi nchini kinyume cha sheria ili kukomesha vitendo hivyo.

Dk. Kigwangalla ametoa tamko hilo jana alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kizi kinachopakana na Pori la Akiba Lwafi lililopo wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa, wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja wilayani humo .


Amesema Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009, Kifungu cha 111 kinaruhusu kutaifisha mifugo na mali itakayokamatwa hifadhini. 


Amesema kwa kipindi cha miezi tisa tangu ateuliwe kuiongoza wizara hiyo amekuwa akitoa msamaha kwa wnanchi wanaakamatwa na mifugo hifadhini jambo ambalo kwa sasa hatofanya tena kwakuwa elimu imeshatolewa vya kutosha.


"Maeneo ya hifadhi sio shamba la bibi lisilokuwa na mwenyewe, ni lazima watu waheshimu sheria za uhifadhi, nawahakikishia tukiwakuta kwenye maeneo ya hifadhi, tutawakamata na kutaifisha mifugo yenu, hakutakuwa na huruma wala msalia mtume" alisisitiza Dk. Kigwangalla.



Wakati huo huo Dk. Kigwangalla ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kuwasilisha ahadi iliyotolewa na Waziri aliyemtangulia ya shilingi milioni 3 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Kizi. Pia ameiagiza mamlaka hiyo kuchangia mabati kwa ajili ya darasa moja katika kijiji hicho ili wananchi wanufaike na faida inayopatikana kwenye uhifadhi. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Mhe. Said Mtanda (kushoto) alipowasili wilayani hapo jana kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja  ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Rukwa.

Dk. Kigwangalla akizungumza katika mkutano huo.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla na Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Said Mtanda (wa tatu kulia) wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkui alipotembelea msitu wa Mfiri ambao ni chanzo cha maji yanayonyesha mji wa Namanyere wilayani Nkasi wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja  kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Rukwa.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kizi wilayani Nkasi wakati wa ziara yake ya siku moja kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Rukwa.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla (wa tatu kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa TAWA, Imani Nkuwi (wa pili kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Pori la Akiba Lwafi alipotembelea maporomoko ya Ntembwa (pichani nyuma) ambayo ni kivutio cha utalii katika pori hilo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya Nkasi mkoani Rukwa jana. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla (wa tatu kushoto waliosomama) na Kaimu Mkurugenzi wa TAWA, Imani Nkuwi (wa pili kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Pori la Akiba Lwafi alipotembelea maporomoko ya Ntembwa (pichani nyuma) ambayo ni kivutio cha utalii katika pori hilo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya Nkasi mkoani Rukwa jana. 

No comments: