ANGALIA LIVE NEWS

Sunday, January 20, 2019

NAIBU WAZIRI MHE. DKT MARY MWANJELWA AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA SEKRETARIETI YA AJIRA

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Xavier M. Daudi akieleza majukumu ya Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi wa Sekretarieti ya Ajira chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kilichofanyika katika ofisi ya Sekretarieti hiyo Magogoni jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (hawapo pichani) alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi ya Sekretarieti hiyo Magogoni jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Baadhi ya watumishi wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na watumishi hao cha kuhimiza uwajibikaji kilichofanyika Magogoni katika ofisi ya Sekretarieti hiyo jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Xavier M. Daudi akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Dkt. Mary Mwanjelwa (Mb) kuhusu namna mfumo wa upokeaji wa maombi ya kazi (Recruitment Portal) na mfumo wa kupanga wasailiwa waliofaulu inavyofanya kazi wakati wa kikao kazi cha Naibu Waziri huyo na Menejimenti ya Sekretarieti ya Ajira alipoitembelea ofisi hiyo kuhimiza uwajibikaji.


JAMES KATUBUKA MWANAMYOTO,
AFISA HABARI,
OFISI YA RAIS-UTUMISHI,
0713 360 813

20/01/2019.



No comments: