Advertisements

Monday, April 15, 2019

Wafanyakazi wa TAA wapigwa msasa na KOICA

  Msimamizi Mwandamizi na Mkaguzi wa Usalama wa anga Sanghoom (Mark) Lim akitoa mafunzo kwa Watendaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kutoka Menejimenti na Vitengo vya Usalama, Uendeshaji na uzuiaji wanyamapori kuhusu masuala ya Usalama katika Viwanja vya Ndege ndani ya Ukumbi wa watu Mashuhuri (VIP) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA TB II).
 Watendaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kutoka Menejimenti na Vitengo vya Usalama, Uendeshaji na uzuiaji wanyamapori  wakiwa katika mafunzo ndani ya Ukumbi wa watu Mashuhuri (VIP) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA TB II).Walioketi mbele kushoto ni Meneja Rasilimali watu na Utawala Bw. Abdi Mkwizu kulia ni Mkurugenzi wa kituo cha Mafunzo ya Anga cha Kiwanja cha Ndege cha Incheon Bw. Chin Hyong, Ryu.
Meneja wa Mafunzo kutoka Kiwanja cha Ndege cha Incheoni Bi. Ji-Yoon Park akitoa mafunzo kwa Watendaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kutoka Menejimenti na Vitengo vya Usalama, Uendeshaji na uzuiaji wanyamapori kuhusu namna ya kuandaa mpango wa kuwaongezea uwezo watendaji katika Viwanja vya Ndege. Mafunzo hayo yamefanyika ndani ya Ukumbi wa watu Mashuhuri (VIP) katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA TB).

Watendaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kutoka Menejimenti na Vitengo vya Usalama, na uzuiaji wa wanyama pori na ndege hai  leo wameshiriki katika mafunzo  ya kuwajengea uwezo wa utendaji katika Viwanja vya Ndege yaliyoandaliwa na KOICA (Korea International Cooperation Agency)  na kutekelezwa na wataalam kutoka Kiwanja cha Ndege cha Incheon kilichopo Korea Kusini ambacho kinaaminika kuwa na ubora nambari moja katika nyanja ya usalama na uendeshaji duniani.

Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa watu mashuhuri Katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere Jengo la pili la abiria (TB II), ikiwa ni  mwendelezo wa mpango wa mafunzo ya miaka mitatu kwa watendaji wa TAA na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA).
Akitoa maelezo kuhusu mafunzo hayo Meneja wa Mafunzo kutoka Kiwanja cha Ndege cha Incheon Bi. Ji-Yoon Park ameeleza kwamba mafunzo hayo ni mwendelezo wa mafunzo ya awali ambapo kwa awamu ya kwanza Mafunzo yalitolewa kwa watendaji takribani 15 kutoka TAA na ZAA na mafunzo haya ni sehemu ya mpango wa mafunzo ya miaka mitatu (2018 – 2020).

Mafunzo haya yatafanyika kwa siku mbili kuanzia leo tarehe 15 Aprili na yatamalizika siku ya kesho16 Aprili nakuendelea huko Zanzibar ambapo yatafanyika katika Mamlaka ya Viwanja vya ndege   Zanzibar.
Katika awamu ya kwanza ya mafunzo haya yalifanyika mwezi Septemba mwaka jana na Watendaji kumi na tano (15) walinufaika na mafunzo haya ikiwa ni (10) kutoka TAA na watendaji na  watano (05) kutoka ZAA.

Ikumbukwe kuwa TAA na ZAA mnamo Juni 2018 waliingia katika makubaliano na KOICA  ya kutoa mafunzo kwa Watumishi  kwa muda wa miaka mitatu ambapo kufikia mwaka 2020 Watumishi 45 watakuwa wamenufaika na mafunzo hayo kutoka Utawala, kada za Ulinzi na Usalama, Tehama, na Uendeshaji.

No comments: