Advertisements

Sunday, October 13, 2019

FAMILIA YAMLILIA JAMES MENSAR, WENGI WAJITOKEZA KATIKA SAFARI YAKE YA MWISHO, YORK, PENNSYLVANIA

Mke wa marehemu Olympia Kullaya Mensar akilia kwa hudhuni na uchungu mbele ya jeneza la mpendwa mume wake James Mensar siku ya Jumamosi Oct 12, 2919 York, Pennsylvania wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Boulding Mortuary nyakati za asubuhi kabla ya kuelekea kanisani. Picha na VIJIMAMBO BLOG
Familia ya marehemu wamejawa huzuni huku Olympia (mwenye miwani) akilia kwa uchungu baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao.
Familia ya marehemu ndugu, jamaa na marafiki wakitoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao.
Mtoto wa marehemu (shati jekundu na nyeusi) akisaidia kubeba jeneza kuingia kanisani kwenye ibada ya kumbukmbu ya mpendwa ya kumwombea baba yake iliyofanyika katika kanisa la katoliki la Mt. Patrick York, Pennsylvania.
Familia ikifuatilia ibada ya kumbukumbu ya misa ya maisha ya James Mensar na kumwombea liyofanyika katika kanisa la katoliki la Mt. Patrick York, Pennsylvania.
 Mke wa marehemu Olympia Kulaya Mensar (kati mwenye miwani) akiwa mwenye huzuni huku akibubujikwa na machozi mara baada ya ibada ya kumwombea mpendwa mume wake kumalizika na ndugu, jamaa na marafiki waliofika kujiandaa kuelekea makaburini katika kumpunzisha mpendwa wetu James Mensar.
Jeneza lenye mwili wamarehemu likipalekwa kwenye gari kulekea makaburini.
Familia ya marehemu wakipata picha ya kumbukumbu katika gari lililobeba jeneza la mwili wa mpandwa wao.
Ndugu, Jamaa na marafiki wakijumuika pamoja na familia katika safari ya mwisho ya mpendwa James Mensar aliyepumzishwa katika makaburi ya Mount Rose, York, Pannsylvania.
WanaDMVna marafiki zao walioenda kwenye maziko ya marehemu James Mensar wakiwa katika picha ya pamoja
Kwa picha zaidi mwanzo mwisho, kuaga mwili, kanisani, maziko na chakula bofya soma zaidi

Mwenye miwani ni aliyekuwa golikipa wa Pamba Paul Rwechungura akisubili kutia saini kitabu cha wageni
Mke wa Paul Rwechungura akitia siani kitabu cha wageni



 Juu nachini ukumbi wa kupata chakula ulivyoonekana

No comments: