Advertisements

Wednesday, April 24, 2024

UMEME KWENYE GRIDI YA TAIFA WAFIKIA MEGAWATI 2,138


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko (Mb)wakati akiwasilisha bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 katika Mkutano wa Kumi na Tano Kikao cha Kumi na Tatu.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko (Mb), ameliambia bunge kuwa katika mwaka 2023/2024 kuwezo wa mitambo ya kufua umeme iliyounganishwa kwenye mfumo wa Gridi ya Taifa umepanda kutoka Megawati (MW) 1,872.1 na kufikia Megawati (MW) 2,138, sawa na ongezeko la asilimia 14.2%.

Mhe. Dkt. Biteko ameyasema hayo leo Aprili 24, 2024 wakati akiwasilisha bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 katika Mkutano wa Kumi na Tano Kikao cha Kumi na Tatu.

No comments: