Monday, August 12, 2024

RAIS WA ZANZIBAR DKT. HUSSEIN MWINYI AJUMUMUIKA NA WANANCHI KATIKA MAZIKO YA ALIYEKUWA KATIBU MTENDAJI WA KAMISHENI YA UTALII ZANZIBAR


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mhe. Juma Duni alipowasili katika Kijiji cha Kikombe Tele Mkoa wa Kaskazini Unguja kuhudhuria Maziko ya aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar Marehemu Walid Fikirini, yaliyofanyika 11-8-2024 Kijijini kwao Kikombe tele.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Viongozi mbalimbali na Wananchi katika Sala ya maiti ya marehemu Walid Fikirini aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, iliyoongozwa na Sheikh.Khamis Abdulhamid, iliyofanyika katika Msikiti wa Kijiji cha Kikombe tele Mkoa wa Kaskazini Unguja 11-8-2024, na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Rashid Hadid Rashid na (kushoto kwa Rais) Babu Juma Duni na Mtoto wa Marehemu Mohammed Walid Fikirini

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Viongozi mbalimbali na Wananchi katika kuitikia dua ya kumuombea marehemu Walid Fikirini aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, baada ya kumalizika kwa sala ya maiti ikisomwa na Sheikh.Khamis Abdulhamid, iliyofanyika katika Msikiti wa Kijiji cha Kikombe tele Mkoa wa Kaskazini Unguja 11-8-2024, na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe. Rashid Hadid Rashid na (kushoto kwa Rais)Mhe.Juma Duni na Mtoto wa Marehemu Mohammed Walid Fikirini
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiweka udongo katika kaburi la marehemu Walid Fikirini aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, yaliyofanyika Kijiji kwao Kikombe Tele Mkoa wa Kaskazini Unguja 11-8-2024.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kutowa mkono wa pole kwa familia ya Marehemu Walid Fikirini aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, alipofika nyumbani kwa marehemu kwa ajili ya kutowa mkono wa pole kwa familia na (kushoto kwa Rais) Mtoto wa marehemu Mohammed Walid Fikirini na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe.Rashid Hadid Rashid
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na familia ya Marehemu Walid Fikirini aliyewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, kuitikia dua ya kumuombea Marehemu, baada ya kutowa mkono wa pole kwa familia ikisomwa na Sheikh.Khamis Abdulhamid na (kushoto kwa Rais) Mtoto wa Marehemu Mohammed Walid Fikirini na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja.Rashid Hadid Rashid

No comments: