Thursday, February 11, 2010

Afrika kusini yamuenzi Mandela

Raia wa Afrika Kusini leo wanaadhimisha miaka ishirini tangu kuachiliwa huru kwa Nelson Mandela.

Sherehe kubwa itakuwa mjini Cape Town ambapo mke wa zamani wa Mandela,Winnie ataongoza maandamano hadi katika gereza ambapo alilitumikia kifungo chake cha mwisho .
Mandela mwenye umri wa miaka 91 anatarajiwa kuonekana hadharani baada ya muda mrefu wakati

atakapo hudhuduria hotuba ya rais kwa taifa leo jioni.
Alitumikia kifungo cha miaka 27 na baada ya kuachiliwa huru aliongoza mazungumzo yaliyopelekea kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza wa demokrasia. Katika uchaguzi huo Mandela alichaguliwa kuwa rais wa Kwanza mweusi nchini Afrika kusini mwaka wa 94.

No comments: