Tuesday, March 26, 2013

MPAMBANO WA MASUMBWI KUFANYIKA JITEGEMEE ULIYOKO WILAYA YA MUHEZA MKOA WA TANGA



IDDY MKWELA
BONDIA Iddy Mkwela wa Dar es salaam anatarajia kuoneshana kazi ya kurushiana makonde na Lucas Ndula wa Muheza wakati wa kusherekea sikukuu za pasaka jumapili ya march 31 katika viwanja vya wazi vya Jitegemee vilivyopo wilaya ya Muheza Mkoa wa Tanga


akizungumza na mwandishi wa habari hizi mratibu wa mpambano huo wa raundi 6 kg,60 bondia wa siku nyingi ambae kwa sasa ni kocha wa mchezo huo Muheza, Chalres Muhilu ' Spins' alisema mpambano huo wa wazi umeandaliwa kwa ajili ya kutoa burudani wilayani hapo na kuhamasisha mchezo wa masumbwi


ambapo kutakuwa na mapambano mengi ya mchezo huo yatakayoanza saa kumi jioni ikiwa kiingilio ni miguu yako tu amewataka wapenzi wa mchezo huo kujitokeza kuangalia mabondia kutoka Dar wakipambana na Muheza pamoja na kutoa rai kujitokeza kwa wafadhili kudhamini mchezo huo unaopendwa na vijana wengi wilayani humo ndio mana tumeamua kuweka katika viwanja vya wazi ili watu wote wajionee wenyewe mchezo wa ngumi unavyo endeshwa katika mazingira magumu


Nae Kocha wa kimataifa wa mchezo huo Rajabu Mhamila 'Super D' aliyepewa jukumu la kwenda na vijana kutoka Dar ili wakalete changamoto na kuleta amasa ya mchezo huo amesema atakwenda na Nassoro Mbwiga atakayemenyana na Bakari Sendekwa katika uzito wa kilo 52 na Iddy Mkwela atakaepambana na Lucas Ndula mpambano wa raundi 6

No comments: