Tuesday, March 12, 2013

VIONGOZI WA DINI NI WADAU MUHIMU KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

 Fatma Gharib Bilar,Katibu  Mkuu wa Wizara ya  Ustawi wa Jamii, Maendeleo, Vijana, Wanawake na Watoto- Serikali ya  Mapinduzi Zanzibar akitoa mada  wakati wa mkutano wa pembezoni ( side- Event) ulioandaliwa na wajumbe wa  Tanzania Visiwani wanaohudhuria Mkutano wa 57 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hali ya Wanawake, katika mkutano huo  ujumbe  huo wa  Zanzibar ulielezea uzoefu wake, mafanikio na changamoto mbalimbali katika kukabiliana na   unyanyasaji wa kijinsia Visiwani  humo. Pamoja na mambo mengine, Katibu Mkuu alisisitiza umuhimu wa  ushiriki wa makundi mbalimbali ya kijamii wakiwamo viongozi wa serikali, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Wabunge, vyama vya hiari, wananchi wa kawaida waume kwa wake na zaidi Viongozi wa Madhehebu yote ya Dini ili kufanikisha  vita hivyo dhidi ya unyanyasaji wa wanawake na watoto. Kushoto kwake ni  Bi Fatma Omar  naye kutoka Zanzibar na kulia ni Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi.
 -Bi. Mira Ihalainen, Mratibu wa Mipango kutoka  Taasisi ya Umoja wa Mataifa, UN- WOMEN ambaye alikuwa mmoja wa wazungumzaji wakuu, katika mazungumzo yake,  Bi Mira alieleza pamoja na mambo mengine kwamba UN- WOMEN itaendelea kufanya kazi kwa  karibu na Serikali ya  Mapinduzi Zanzibar na  Serikali ya Muungano ikiwa ni pamoja  na kutoa misaada mbalimbali ya kiufundi na kitaalam katika shughuli zote zinazolenga kumkomboa  mwanamke na mtoto wa kike. kulia kwake ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ( Tanzania Bara), Bi. Kijakazi Mtengwa  akifuatilia majadiliano hayo na kushoto kwa  Mira ni  Afisa Ubalozi, Modest Mero aliyekuwa mratibu wa  wa majadiliano.

Na Mwandishi Maalum
Fatma Gharib Bilar, Katibu Mkuu , Wizara ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto, katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, amesema, viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini, wanayo nafasi kubwa na ya muhimu katika kukabiliana na unyanyasaji dhidi ya wanawake na watoto wa kike.

Ameyasema hayo jana jumatatu wakati ujumbe wa Tanzania Visiwani, unaoshiriki mkutano wa 57 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu Hali ya Wanawake ( CSW) ulipoanda mkutano wa pembezoni ( side event) kwa lengo la kubadilishana na washiriki wengine uzoefu wao , mafanikio na changamoto wanazokabiliana nazo katika kushughulikia unyanyasaji wa kijinsia Tanzania Visiwani.

Mkutano huo wa pembezoni na ambao ulivutia washiriki wengi mada yake ilikuwa “Vunja ukimya, unga mkono, juhudi za sekta mtambuka katika kuzuia na kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia, uzoefu wa Zanzibar”.
Kwa habari zaidi na picha, bofya read more
Akiwa msemaji mkuu wa mkutano huo,  Katibu Mkuu, Fatma Bilar ameeleza kwamba  kwa  uzoefu wa wao  (Zanzibar) wamebaini kwamba, ili juhudi hizo ziweze kufanikiwa,  mbali ya ushiriki wa viongozi wa serikali na wadau wengine, viongozi wa madhehebu ya dini ni kundi ambalo  lina umuhimu wa kipekee.
“ harakati zetu zinahusisha makundi mbalimbali ya kisekta,  zikiwazo  wizara, idara na taasisi mbalimbali achilia mbali viongozi wakuu wa serikali, lakini tumetambua kwamba hakuna dini yoyote ile inayohubiri ukatili dhidi ya wanawake, na kwa sababu hiyo tunaamini kwamba viongozi wa madhehebu yote ya dini wanapashwa kushirikishwa na kushiriki kikamilifu katika  juhudi hii” akasisitiza Katibu  Mkuu.
 Na kuongoza kwamba,   viongozi hao wa madhehebu ya dini bila ya kujali kama ni waislamu au wakristo wote wamekuwa wakijitahidi kuunga mkono harakati hizo kwa kuwaelimisha  waumini wao  kuhusu madhara ya unyanyasaji wa kijinsia.
Akabainishwa kuwa  ilichukua juhudi  nyingi  ukiwamo utafiti kubaini kwamba Zanzibar kulikuwa na tatizo kubwa la unyanyasaji na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Akasema  tafiti hizo ndizo zimewafumbua macho hata viongozi wa serikali na mamlaka  mbalimbali na  hivyo kuanza kuchukua hatua  za kulikabili tatizo hilo.
Akaainisha  juhudi  mbalimbali na baadhi ya mafanikio  yakiwamo yale ya kuanzisha makazi salama ya kuwahifadhi waathirika . Ingawa ambayo ingawa alikiri kwamba bado kuna changamoto nyingi za uhaba wa raslimali fedha, wataalamu na kazi kubwa ya kubadili fikra na mitazamo ya watu kuhusu suala zima la ukatili wa kijinsia.
Washiriki wa mkutano huo wa pembezoni  baada ya maelezo ya  Katibu Mkuu walipata nafasi ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi zaidi. Na Maswali yote pamoja  ufafanuzi huo yalijibiwa kwa Ufasaha na Katibu  Mkuu pamoja na wajumbe aliofuatana nao.
 washiriki wakifuatilia mkutano
 Sehemu ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo wa pembezoni  ulioandaliwa na ujumbe wa Tanzania Visiwani.
mjumbe akiuliza swali
 wajumbe walijitokeza kwa wingi kuja kujisikilizia uzoefu wa wataalamu hawa kutoka Tanzania Visiwa
 wajumbe wengine wakifuatilia mada
 isiwe taabu wengine waliamua kujikalia chini.
 Katibu Mkuu akiendelea kujibu mswali kutoka kwa washiriki waliokuwa bado  na hamu ya kujifunza kutokana na uzofu wa Zanzibar.

No comments: