ANGALIA LIVE NEWS

Monday, March 24, 2014

MAELEZO YA KUFADHILI FILAMU ZA KISWAHILI KWENYE ZUKU TV IDHAA YA SWAHILI MOVIES


Televisheni ya Zuku inataka kufadhili filamu za kiswahili ambazo zitarushwa kupitia
idhaa ya Zuku Swahili Movies, ikiwa ni idhaa pekee, ambayo, imetabaruku
kuonyesha filamu za kiswahili zenye ubora wa hali ya juu kwa masaa ishirini na nne
kila siku.

Idhaa ya Zuku swahili Movies ni idhaa ambayo inaonyesha filamu zenye uhondo na
ambazo zimetengenezwa kwa ubora wa kuonyeshwa kwa kila rika na kukidhi
mategemeo ya kila mtazamaji wa Afrika mashariki. Idhaa hii inatafuta kukidhi haja
kubwa ya watazamaji ambao wanataka kuona filamu zilizotengenezwa na waafrika,
na mandhari ya kiafrika na kujipa fahari kwa ubora wa kazi zake.

Tunatafuta kazi nzuri, zenye uhamasa, za kipekee, zenye uhalisia na ambazo zitaleta
muonekano wa aina yake kwa televisheni ya afrika mashariki.

Waigizaji lazima wawe na ufasaha mzuri katika lugha fasaha ya kiswahili na pia
wanaweza kuwashirikisha wahusika kutoka bara la Afrika.


MAUDHUI
Sinema/Filamu za kiswahili endelevu lazima zizingatie yafuatayo;

 Hadithi za kusisimua

 Hadithi zenye kufikirika na kuhamasisha

 Mwendelezo imara

 Wahusika wasiosahaulika

 Mandhari ya kuvutia

 Muonekano wa kipekee

 Kuwa ya asili na ya kipekee

 Kuburudisha

PENDEKEZO
Mapendekezo yaweze kulenga familia au watazamaji waliokomaa na lazima iwe na
maelezo yafuatayo:

1. Muhtasari

2. Mswada

3. Waigizaji na maelezo yao

4. Mtazomo wa filamu

5. Ratiba ya utayarishaji wa filamu

6. Watayarishaji wa filamu wakuu

7. Bajeti

MAELEZO YA ZIADA
LUGHA: Kiswahili. Filamu itatafsiriwa na maandishi ya lugha ya
MUDA: Dakika tisini kwa mia moja na ishirini
HADHIRA INAYOLENGWA: Filamu iwe na rufaa ya kimataifa
UTANZU: Filamu kamili

UTARATIBU WA UCHAMBUZI
1# Baada ya kufanikwa kutuma pendekezo yako utapokea taarifa kupitia barua
pepe ikiidhinisha risiti

2# Pendekezo yako ita tathminiwa na jopo la majaji walio chaguliwa na mhariri
kuwaagiza

3# Kama pendekezo yako inapatana na mahitaji yetu, pendekezo yako itafanywa

tathmini zaidi na katika hatua hii unaweza ombwa kufika ofisi zetu kwa kikao

cha kuuza hoja zako zaidi.

4# Jopo la majaji litafanya ukaguzi zaidi wakizingatia lami yako na kuandaa

orodha ya mwisho ya mapendekezo yaliyofanikiwa

5# Basi utapokea barua pepe ikikutaarifu kama au la, pendekezo yako

imechaguliwa kwa ajili ya maendeleo zaidi.

TAARIFA NYINGINE MUHIMU
UTOAJI MUUNDO: Unaweza kutuma filamu kwa kutumia hard drive,
ANWANI YA KAMPUNI: Eneo kamili na anwani ya kampuni yako.
HATI TAMBULISHO: Mtaala vitae ya wafanyikazi muhimu amabo watakuwa
MAREJELEO: Filamu ulizozifanya ndani ya miaka mitatu iliyopita
MAWASILIANO: Jina na namba ya mtu muhimu ambaye tutawasiliana
kingereza filamu yenyewe iwe na kipengele uwiano 16:9 kwa ajili ya mradi huu naye.

TAREHE YA MWISHO YA KUWASILISHA: Aprili tarehe 17, mwaka 2014

MWISHO WA UAMUZI: Mei tarehe 30, mwaka 2014

UZINDUZI WA FILAMU: Januari mwaka 2015

KUWAASILISHA MAELEZO:
Mapendekezo lazima yatumwe kwa:

Mhariri kuwaagiza,
Wananchi Programming ltd
Gateway Business Park, Block E, Mombasa Road
P. O. Box 10286-00100,Nairobi, Kenya

Barua Pepe: zukuswahilimovies@ke.wananchi.com

 Pendekezo kutoka nchi karibu na kanda ya Afrika Mashariki zinakubalika.

No comments: