Advertisements

Monday, April 17, 2017

SAMIA : VIJANA WANA KASI YA 4G WAPEWE NAFASI YA KUKIONGOZA CHAMA

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongea na wanachama wa tawi la Muungoni mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi ya Tawi la Muungoni lililopo Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea taarifa ya ujenzi ya shule ya awali ya Watoto Kajengwa, Makunduchi kutoka kwa Mhandisi Riziki Jescha Salim, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiondoka eneo inapojengwa shule ya watoto ya awali iliyopo Kajengwa, Makunduchi mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wakina Mama wanachama wa CCM waliojitokeza kwenye mkutano wake na wajumbe wa kamati za siasa kuanzia matawi mpaka ngazi ya mkoa.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia kwenye mkutano wake na wajumbe wa kamati za siasa kuanzia tawi mpaka mkoa ambapo aliwaambia wajumbe hao kuwa ni wakati wa kukiimarisha Chama sasa na kutoa elimu ya Itikadi kwa wanachama.
Sehemu ya wajumbe 535 waliohudhuria mkutano wa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye amehitimisha ziara yake ya kuimarisha chama katika Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wajumbe wa kamati za siasa kuanzia matawi mpaka mkoa kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari ya Makunduchi ambapo aliwasihi wazee kutoa elimu kwa vijana katika historia ya Mapinduzi kisha kuwapa nafasi vijana zaidi ambao kasi yao ni ya 4G.
Vijana wa Makunduchi wakionesha juu picha za Viongozi wao wakati wa ziara ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

No comments: