Advertisements

Monday, September 23, 2019

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kuwaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bw. Loata Sanare kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bw. Alphayo Kidata kuwa Katibu Tawala mkoa wa Mtwara katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Ally Possi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Mussa Lulandala kuwa Balozi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Viongozi mbalimbali walioapishwa wakila Kiapo cha Uadilifu kwa Viongozi wa Umma Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Viongozi wengine wa Serikali Kuu katika picha ya pamoja na viongozi waliopishwa Ikulu jijini Dar es Salaam.

No comments: