Advertisements

Saturday, April 17, 2021

RAIS DK.MWINYI AJUMUIKA NA WAUMINI WA KIISLAM KATIKA SALA YA TARAWEKH MSIKITI WA IJUMAA MIEMBENI JIJINI ZANZIBAR

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Msikiti wa Ijumaa Miembeni Jijini Zanzibar alipowasili kwa ajili ya Ibada ya Sala ya Isha na Tarawekh, iliofanyika katika msikiti huo jana usiku 16-4-2021.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini wa Kiislam katika Sala ya Tarawekh, ikiongozwa na Ust.Kassam Seif na (kulia kwa Rais) Naibu Imamu wa Msikiti wa Miembeni Sheikh.Fahim Hafidh na (kushoto kwa Rais) Katibu wa Mufti Mkuu Sheikh Khalid Ali Mfaume, wakiwa katika Sala ya Tarawekh iliofanyika katika msikiti wa Ijumaa Miembeni Jijini Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume (kushoto kwa Rais) na (kulia kwa Rais) Naibu Imani waMsikiti wa Ijumaa Miembeni Sheikh Fahim Hafidh, wakiitikia dua baada ya kumalizaka kwa Sala ya Tarawekh iliofanyika katika msikiti huo jana usiku 16-4-2021.
WAUMINI wa Dini ya Kiislam wakiitikia dua ikisomwa na Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Khalid Ali Mfaume (hayupo pichani) baada ya kumalizika kwa Sala ya Tarawekh iliofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Miembeni Jijini Zanzibar jana usiku 16-4-2021.(Picha na Ikulu)

No comments: