Friday, January 26, 2024

MAKATIBU WAKUU WA VYAMA 6 VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA WASAINI MAKUBALIANO YA USIMAMIZI WA SHULE YA MJNLS


Makatibu Wakuu wa Vyama Sita Marafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, wakionesha nakala ya Katiba ya Usimamizi na Uendeshaji wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), baada ya kutia saini, eneo la Kwa Mfipa, Kibaha, mkoani Pwani, Tanzania.
Kuanzia katikati kwenda kulia ni Komredi Dk. Emmanuel John Nchimbi, Katibu Mkuu wa CCM (Tanzania), Prof. Marcelina Chijoriga, Mkuu wa Shule ya MJNLS, Komredi Fikile Mbalula na Katibu Mkuu wa ANC (Afrika Kusini) na Komredi Francisco Mucanheia, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO (Msumbiji). Kuanzia kwa Dkt. Nchimbi kwenda kushoto ni Komredi Obert Moses Mpofu, Katibu Mkuu wa Chama cha ZANU- PF (Zimbabwe), Komredi Sophia Shaningwa Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO (Namibia) na Komredi Manuel Domingos Augusto, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa MPLA (Angola).
Makatibu Wakuu wa Vyama Sita Marafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, wakisaini Katiba ya Usimamizi na Uendeshaji wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), eneo la Kwa Mfipa, Kibaha, mkoani Pwani, Tanzania.

No comments: