Wednesday, January 24, 2024

TRUMP AMGARAGAZA NIKKI HALEY KWENYE UCHAGUZI WA CHAMA CHA REPUBLICAN HUKO NEW HAMPSHIRE


Hakuna kinachoonekana kumzuia Donald Trump anapokaribia uteuzi wake wa tatu mfululizo wa chama cha Republican  Hugo Marekani.


Rais huyo wa zamani jana Jumanne alikua mgombea wa kwanza wa chama cha Republican asiyekuwa madarakani kushinda kwa kishindo ngwe  ya uteuzi wa rais, akiongeza ya mchujo wa New Hampshire kwenye uchaguzi mkuu wa Iowa kuanzia wiki iliyopita, na akafikia ukingo wa kurudiana na Rais Joe Biden. .


Trump ameweza kuvuka ngwe ya uwanja muhimu wa mapambano  wa chama cha Republican maarufu kama GOP kwa kasi ya kushangaza.


Licha ya tuhuma ya uhalifu na ya shambulio lake dhidi ya demokrasia mnamo Januari 6, 2021, Trump anaonekana kufanikiwa kukiweka  chama chake karibu naye zaidi kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa katika chaguzi za msingi za kisasa za Marekani


Hata hivyo, inasemekana kwamba badala ya kusherehekea Trump alitumia Jumanne usiku kucha akilaani kwa hasira, vyanzo vilimwambia Kaitlan Collins wa CNN, kwa sababu mpinzani wake pekee aliyesalia wa GOP, Gavana wa zamani wa South Carolina, Nikki Haley, Magoma kukubali yaishe na kumwachia yeye Nafasi ya kusaka uteuzi wa GOP agombee.


Licha ya kushindwa kupata ushindi dhidi ya rais huyo wa zamani katika jimbo hilo ambaye anamfaa zaidi katika kugombea kwake, alisisitiza kuwa ataendelea, akipinga shinikizo kubwa kutoka kwa kambi ya Trump kujiuzulu na kuahidi kushiriki katika kile kinachoonekana kama vita kubwa ndani yake. 


Trump alimkosoa Haley hadharani na kwa faragha na kuwasihi wasaidizi wake wa kisiasa kufanya mashambulizi dhidi yake, Collins aliripoti.

No comments: