Friday, July 5, 2024

WADAU WA USAFIRI WA ANGA WAENDELEA KUJIPAMBANUA KATIKA MAONESHO YA SABASABA

 Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka TCAA Bw. Teophory Mbilinyi, ametembelea jengo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (Aviation House) lililopo ndani ya viwanja vya Sabasaba na kujionea namna wananchi wanaofika katika banda hilo wanavyopatiwa huduma, TCAA inashiriki maonesho ya 48 ya Kimataifa ya biashara katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam.

Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka TCAA Bw. Teophory Mbilinyi akisaini kitabu alipotembelea jengo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (Aviation House) lililopo ndani ya viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka TCAA Bw. Teophory Mbilinyi akipata maelezo kutoka kwa Mkufunzi Mkuu wa kitengo cha Uongozaji Ndege, Godlove Longole alipokuwa anaelezea kuhusu Chuo cha Usafiri wa Anga nchini(CATC) kinachomilikiwa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka TCAA Bw. Teophory Mbilinyi akipata maelezo kutoka kwa Afisa Kitengo cha Sheria Massa Mumburi kuhusu namna wanavyopokea malalamiko mbalimbali yayotolewa na wananchi kuhusu Usafiri wa Anga alipotembelea jengo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (Aviation House) lililopo ndani ya viwanja vya Sabasaba  katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka TCAA Bw. Teophory Mbilinyi akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mipango na Takwimu kutoka TAA Edward Kimaro alipotembelea jengo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (Aviation House) lililopo ndani ya viwanja vya Sabasaba  katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka TCAA Bw. Teophory Mbilinyi akipokea zawadi kutoka kwa Afisa Uhusiano kutoka TAA Mariam Lussewa alipotembelea jengo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (Aviation House) lililopo ndani ya viwanja vya Sabasaba  katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Huduma za Mamlaka TCAA Bw. Teophory Mbilinyi akipata maelezo kutoka kwa Afisa Masoko na Biashara  ATCL Jerry Ngewe alipotembelea jengo la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (Aviation House) lililopo ndani ya viwanja vya Sabasaba  katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam.

 

No comments: