Advertisements

Friday, August 31, 2012

MKUTANO WA DICOTA CHICAGO IJUMAA AUG 31, 2012

Felicia Davis ambae alileta salaam kutoka kwa Meya wa Chicago, Rahm Emanuel ambae ametangaza Ijumaa Aug 31, 2012 kuwa Siku ya Mtanzania Chocago.
Rais wa DICOTA Dr. Ndaga Mwakabuta akiongea machache kabla hajamkaribisha Balozi wa Tanzania Nchini Marekani na Mexico, Mhe. Mwanaidi Maajar.
Balozi wa Tanzania Nchini Marekani akiongea machache kabla hajamkaribisha mgeni rasmi Mstaafu Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Aman Karume.
Mgeni rasmi mkutano wa DICOTA 2012 Rais Mstaafu awamu iliyopita Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Aman Karume akiongea machache kabla ya kuufungua mkutano rasmi.
Rais mstaafu wa serukali ya mapinduzi Zanzibar, Mhe. Aman Karume akimkabidhi zawadi Felicia Davis baada ya kuufungua mkutano.
Mhe. Aman Karume na Mkewe, Mkewe mama Karume katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania Nchini Marekani, Mhe. Mwanaidi Maajar (kushoto)
 Mgeni rasmi wa mkutano wa DICOTA Mhe. Aman Karume Rais mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akisalimiana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu
 Mhe. Aman Karume akisalimiana Viongozi wa DICOTA
 Mhe. Aman Karume akisalimiana na maafisa Ubalozi wa Tanzania Nchini Marekani
 Mhe. Aman Karume Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akigakua vibanda vya Wajasilia Mali kwenye mkutano wa DICOTA unaoendelea Chicago, IL hapa akiwa kwenye banda la mama mitindo Asya Idarous Khamsin.
 Mhe. Aman Karume Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akisalimiana na mwanamuziki wa kizazi kipya Peter Msechu ambae nae alikua na kibanda chake.
kwa picha zaidi bofya read more

No comments: