Advertisements

Friday, December 7, 2012

NDUGU NA MARAFIKI KUTOKA DC NA MA WA FAMILIA YA MAREHEMU ISMAT STEINER ALIEFARIKI DEC 6 AZIKWA KATIKA MAKABURI YA ROSE HILL MEMORIAL PARK, PUTNAM VALLEY,NY BAADA YA SALA YA IJUMAA.

 
Mh.Balozi Tuvako Manongi wa Tanzania Mission,NY akiongea machache baada ya mazishi ya mume wa alie kuwa mfanyakazi wa Tanzania Mission, Ny Ms Masikini Steiner. Ms Masikini Steimer ameitumikia Tanzania Mission, NY kwa zaidi ya miaka 20 na kastahafu hivi karibu. Mr Ismat Steimer aliefariki Dec 6 na kuzikwa katika makaburi ya Rose Hill Memorial, Putnam Valley, Ndugu jamaa na marafiki wa New York na sehem nyingine kama Boston, MA, na Maryland lichaaya kuwa na mvua za rasha rashakibaridi lakini haikuzuia watu kuhuzuria mazishi hayo. Mazishi yalifanyika baada ya sala ya Ijumaa  , sala hiyo ilifanyika Westchester Muslim Center,Mt Vernon, NY. M/Mungu amlaze mahala pema amen.

 Mh. Balozi Manongi akiweka udongo katika kaburi la  marehem, Mr Steiner, kwa picha zaidi bofya read more.

 Kila mja ataonja mahuti hapa ndo ilikuwa safari ya mwisho ya Mr Steiner
 Ingawa kulikuwa na mvua lakini ndugu na marafiki walishirikiana kwa moyo mmoja kuhustili mwili wa mpendwa wao kama unavyoona wakiweka udongo. 
 Mkuu wa wilaya ya Springfield, MA alikuwepo nae makaburini hapo
 Mh. Balozi Manongi na naibu msaidizi wake Mh. Mwinyi walikuwepo nao sambamba na ndugu na marafiki makaburini hapo.
 Maustadhi wakisoma duwa baada ya mwili wa marehemu kustiriwa ardhini makaburini hapo,Ustadhi Hajji, Abbas na Hamza Mandia kutoka Brooklyn, NY
 Bwana Isaac Kibodya akisikiriza duwa iliyo kuwa inasomwa na maustadhi makaburini hapo

 Akina mama nao walikuwepo sehemu ya mazishi kama unavyo ona sambamba na mjane wa marehem
 Ms Masikini Steiner mke wa marehemu akifarijiwa na akina mama wenzie waliofika makaburini hapo
 Ndungu, marafiki wa familia ya marehemu wakiondoka makaburini hapo baada ya mazishi
Licha ya mvua na kibaridi ndugu na jamaa walikuwa pamoja hadi safari ya mwisho ya marehemu Mr Steiner mwenyezi mungu amlaze mahala pema amen.

No comments: