Advertisements

Monday, March 18, 2013

WANACHUO WAASWA KUHUSU USHOGA MBEYA

Mhasamu askofu wa katoriki jimbo Mbeya Ask. Evaristo Chengura
WANAFUNZI wa vyuo vikuu ambao ni waumini wa dhehebu la Katoliki mkoani Mbeya wamedai kuwa wamekukipambana na changamoto ya ushawishi wa kujihusisha na ushoga vyuoni kwao.
Wakisoma risala yao mbele ya Mhasamu askofu wa katoriki jimbo Mbeya Ask. Evaristo Chengura katika semina kwa muungano wa wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi za elimu waumini wa Katoriki Mbeya (MUCCASA), walisema kuwa wamekuwa wakikabiliana na changamoto ya ushoga vyuoni.
Akisoma risala hiyo Mwenyekiti wa Muccasa, Alfred Nditi alisema kuwa wamekuwa wakikabiliana na changamoto ya uhamasishwaji wa masuala ya ushoga unaoshawishiwa na mataifa makubwa ya ughaibuni.
Alisema ushawishi huo umekuwa ukiwalenga vijana hasa walio katika vyuo mbalimbali vya elimu ya juu hapa nchini ili wajikite katika uovu huo.
“Ushoga umekuwa ukihamasishwa na mataifa mbalimbali hasa yale makubwa ya Ughaibuni na ukitulenga vijana tulio kwenye vyuo vikuu hapa nchini,” Alisema Nditi.
Alisema ili kupambana na changamoto hizo wanamatarajio ya kupinga ushoga kwa kauli moja ili kukidhi dhana ya Mungu na uumbaji wake.
Nditi aliongeza kuwa upingaji wa ushuga utakuwa ni wa kauli moja kwa wanaMuccasa na kuhakikisha dhana ya Mungu ina heshimiwa na thamani ya binadamu ienziwe.
Naye Askofu Chengula alisema kuwa ushoga umekuwa ukipingwa sana na viongozi wote wa dini lakini umekuwa ukiendeshwa chini chini na baadhi ya watu.
“Ushoga unapigiwa sana kelele lakini kumekuwa na watu wanaouendesha chini kwa chini na kwa siri kubwa katika maeneo mbalimbali na hasa katika vyuo,” alisema Ask. Chengula.
Aliwaasa wanamuccasa kwu kuwaonya wale watakao wakuta wanakijihusisha na mambo hayo machafu na kuwashawishi kuachana na matendo hiyo.
Alisema ni vema wakawapatia elimu juu ya kuachana na mambo hayo na kuwaeleza madhala na ubaya wa Ushoga katika maisha yao kwani wengine wanakuwa wameathirika kisaikolojia.
Semina hiyo kwa wananchuo ililenga kuwaelimisha wanachuo hao juu ya imani yao na jinsi ya kusimama katika imani ambapo ilihuzuriwa na wanachuo kutoka katika vyuo mbalimbali vya Mkoani Mbeya.
Muccasa ni muunganiko wa wanachuo kutoka katika vyuo vikuu na taasisi za Mkoani hapa na inajumla ya matawi 20 ya wanamuccasa.
Kwa hisani ya Furaha Elimitaa blog

No comments: