Advertisements

Monday, September 8, 2014

Mshitakiwa wa Ugaidi Aonyesha Alivyolawitiwa na Polisi Mahakamani

MMOJA wa watuhumiwa wa ugaidi katika kesi inayomkabili Kiongozi wa Jumuiya za Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu (JUMIKI) Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmed (43), amevunja ukimya mahakamani baada ya kuonyesha suruali ilivyolowa kwenye makalio akisema ni madhara ya kulawitiwa na kuingizwa miti na polisi.
Mshtakiwa huyo, Salum Ally Salum, aliamua kufanya hivyo jana ili kuithibitishia mahakama kile walichodai ni unyama waliotendewa na polisi wakati wakihojiwa.

“Mheshimiwa hakimu, angalia (anageuka na kuinua suruali katika eneo la makalio), haya ndiyo madhara niliyopata kwa kuingiliwa nyuma na kuingizwa jiti,” alidai.

Baada ya mshtakiwa huyo kuzungumza, Hakimu Hellen Riwa alimshauri kutoa taarifa kwa uongozi wa Magereza ili aweze kupata matibabu ya haraka kwani akiendelea kukaa hivyo anaweza kupata madhara makubwa.

No comments: