Ni stori ya kusikitisha sana! Aliyekuwa Mbunge wa Kilwa Kaskazini mkoani Lindi kwa ‘leseni’ ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kati ya mwaka 2005 hadi 2010, Dk. Samson Mpanda, amesimulia jinsi alivyopata upofu akiwa kwenye nafasi yake ya ubunge, tatizo ambalo lilimuanza mwaka mmoja tu baada ya kuchaguliwa na kuanza kuhudhuria vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma.
Akisimulia mkasa huo wa kuumiza mbele ya waumini wa Kanisa la The Revelation Church chini ya Nabii Yaspi Bendera lililopo Buza-Kipera jijini Dar, Dk. Mpanda aliyeongozana na Diwani wa Kata ya Kijichi, William Ntiwundi ambaye ni kaka yake, alidai kwamba alifika kanisani hapo baada ya kuuguza macho yake katika hospitali mbalimbali bila mafanikio.
Alieleza kwa masikitiko kwamba ulipofika uchaguzi mwingine ilibidi aachie ngazi ambapo nafasi yake ilichukuliwa na Multaza Mangungu (Mbunge-CCM) anayeitumikia hadi sasa.
Wanahabari wetu walishuhudia tukio la mbunge huyo akiombewa na Nabii Yasip ambaye alisema kuwa Dk. Mpanda alifanywa kipofu kutokana na roho mbaya za watu huku akiahidi kumuombea na hatimaye kurudia hali yake.
GPL
No comments:
Post a Comment