Advertisements

Tuesday, February 3, 2015

Mhe. Rais Kikwete ampokea rasmi Rais Gauck-Ikulu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimpokea rasmi Rais wa Ujerumani, Mhe. Joachim Gauck katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam. 
Rais Kikwete akiwa ameongozana na mgeni wake Rais Gauck mara baada ya kumpokea. 
Rais Kikwete na Rais Gauck wakipata heshima ya nyimbo za mataifa yao ikiwa ni sehemu ya mapokezi ya Rais Gauck. 
Kikosi cha jeshi kikipiga mizinga 21 kwa heshima ya Rais Gauck 
Rais Gauck akikagua Gwaride la Heshima 
Sehemu ya waandishi wa Habari wakiwa kazini 
Sehemu ya umati wa watu waliofika Ikulu kwa ajili ya mapokezi ya Rais Gauck 
Rais Gauck akisalimiana kwa furaha na wanafunzi waliofika Ikulu kumpokea 
Picha ya pamoja 
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mama Schadt, Mke wa Rais wa Ujerumani 
Mhe. Rais Kikwete akimpatia Rais wa Ujerumani, Mhe. Gauck zawadi ya picha ya michoro maarufu nchini ya "Tingatinga" 
Rais Kikwete akifurahia zawadi aliyokabidhiwa na Rais Gauck 
Rais Kikwete na Ujumbe wake wakiwa kwenye mazungumzo rasmi na Mhe. Gauck na Ujumbe wake (hawapo pichani) Kulia kwa Rais ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal na kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Memnbe (Mb.). Wengine ni Prof. Jumanne Maghembe (wa tano kushoto) , Waziri wa Maji. 
Rais Gauck (wa tano kulia) na Ujumbe wake wakati wa mazungumzo rasmi 
Mazungumzo yakiendelea 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (wa pili kushoto) akiwa na Maafisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo rasmi kati ya Rais Kikwete na Rais Gauck (hawapo pichani) Picha na Reginald Philip.

No comments: