Advertisements

Friday, May 1, 2015

SHEREHE ZA MEIMOSI ZILIYOFANA MKOANI KILIMANJARO


Wafanyakazi wa Shirika la Umeme(TANESCO) mkoa wa Kilimanjaro wakipita na gari lao mbele ya mgeni rasmi katika sherehe za Mei Mosi zilizofanyika katika uwanja wa Chuo Kikuu chaUshirika mjini Moshi. 

Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCLwakipita katikamaonesho ya Mei Mosi 

Chuo cha wauguzi Kibosho pia walipita mbele ya mgeni rasmi kuonesha nini wanafanya katika sherehe hizo za Meio Mosi. 
Mtafiti kutoka kituo cha utafiti wa zao la Kahawa ncini cha TACri ,Jeremiah Magesa akitoa maelezo mbele ya mgeni rasmi namna ambayo kituo hicho kinavyo saidia katika upatikanaji wa mbegu bora ya zao la Kahawa. 

Moja ya mtambo inayotumika kunyunyiza dawa katika Kahawa ikioneshwa mbele ya mgeni rasmi. 
Kampuni ya Swissport pia walikuwepo kuonesha kazi wanayofanya katika viwanja vya ndege. 

Kassim Mwinyi akitoa maelezo kuhusu kampuni ya Panone inavyosaidia katika utoaji wa huduma ya mafuta. 

Mwakilishi wa kampuni ya Bia Tanzania ,Pudensiana akitoa maelezo kuhusu kampuni hiyo. 

Magari ya kampuni ya TBL yakipita mbele ya mgeni rasmi. 

Baaadhi ya wa wafanyakazi wakifuatilia maonesho hayo. 

Afisa Masoko wa Hifadhi ya taifa ya mlima Kilimanjaro (KINAPA)Antypas Mgungusi akitoa maelezo juu ya ofa iliyotolewa na hifadhi hiyo ya kupanda mlima Kilimanjaro hadi kilele cha Shira kwa gharama za Kiasi cha sh 25.000ikijumuisha kiingilio hifadhini,usafiri wa kwenda na kurudi ofa inayotaraji kuanza rasmi Mei 15 mwaka huu. 
Halmashauri ya manispaa ya Moshi wakionesha shughuli mbalimbali wanazofanya pamoja na kikombe cha mshindi wa pili wa usafi. 
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi ,Jafary Michael akikabidhi kikombe cha ushindi wa nafasi ya pili katika usafi pamoja na cheti kwa mgeni rasmi kaimu mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Novatus Makunga katika shrehe za Meio mosi zilizofanyika katika uwanja wa chuo kikuu cha Ushirika. 
Bodi ya Kahawa Tanzania TCB pia walikuwepo katika sherehe hizo. 

Watengenezaji wa Highlife Gin pia waipita kutangaza bidhaa zao mele ya mgeni rasmi. 

Kampuni ya SBC watengenezaji wa kinywaji cha Pepsi na jamii yake pia walipita kuonesha vinywaji vinavyo tengenezwa nakampuni hiyo. 

Kampuni ya Sukari ya TPC ilitia fora baada ya kuingiza mitambo yake inayotumika katika kilimo,kunyunyiza dawa pamoja na kupakia miwa wakati wa uvunaji. 

hata hivyo vijana walikosa uvumilivu wakalazimka kukimbilia miwa iliyoachwa uwanjani hapo kwa ajili ya maonesho. 

Wafanyakazi wakiimba wimbo wa Solidarity katika sherehe hizo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii na Vijimambo Kanda ya Kaskazini. 

No comments: