Advertisements

Thursday, July 30, 2015

MABAKI YA NDEGE YANAYOSEMEKANA NI YA NDEGE YA MALAYSIA

Ndege ya Malaysia iliyopotea yaBoing 777 , MH370

Mamlaka ya usafirishaji nchini Ufaransa imesema inachunguza mabaki ya ndege ya yanayodaiwa kupatikana ndani ya Bahari ya Hindi yanachunguzwa ili kubaini kama ni ya ndege ya Malaysia ya MH370 iliyopotea bila kuwa na taarifa zozote kwa muda mrefusasa.

Taarifa kutoka Marekani zinasema wachunguzihao ambao wameona picha za mabaki hayo wana uhakika mkubwa kwamba ni ya ndege hiyo ya Malaysia ambapo mabaki hayo ni sehemu ya bawa la ndege.

Hata hivyo, Wataalamu wa Ufaransa wanasema ni mapema mno kutoa uhakika kwamba mabaki hayo ni lazima yatakuwa ya ndege ya Malaysia aina ya Boeing 777 ambayo kupotea kwake kumeleta gumzo la kidunia.

Watu wapatao 239 waliokuwa wakisafiri na ndege hiyo walipoteza maisha.

Akizungumza mjini New York Marekani, Waziri wa Usafirishaji wa Malaysia Liow Tiong Lai amesema nchi yake imetuma wataalamu zaidi kuchunguza mabaki hayo.

"Tunahitaji kuthibitisha" amekaririwa akisema Waziri Lai,na kusisitiza kuwa kwa vyovyote vile, mabaki yaliyopatikana yanahitaji kuhakikishwa kabla ya kuthibitisha zaidi kama ndio hasa mabaki ya MH370.

BBC

No comments: