Advertisements

Friday, July 31, 2015

TANZIA

Marehemu SACP Aneth Laurent

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, John Casmir Minja anasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza - SACP Aneth Laurent kilichotokea jana Julai 30, 2015 katika Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza.

Kamishna Jenerali wa Magereza anatoa pole kwa Watumishi wote wa Jeshi la Magereza nchini, familia na wale wote walioguswa na msiba huu kwa namna tofauti tofauti.

Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na familia ya Marehemu linaendelea kuratibu shughuli za msiba ambapo mwili wa Marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwa ndege kutoka Mwanza kuja Jijini Dar es Salaam na taarifa za mazishi zitatolewa baadaye baada ya taratibu zote kukamilika.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi Amina.

1 comment:

Anonymous said...

Bwana ametoa na yeye amechukua. Jina lake lihimidiwe. Upumzike kwa Amani dada Aneth.