VIJIMAMBO

ANGALIA LIVE NEWS

Saturday, March 19, 2016

MAKONDA ADAI HATA AKIFA AMESHAFANIKIWA, ATANGAZA VITA KALI NA WAUZA UNGA


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
MAKONDA ADAI HATA AKIFA AMESHAFANIKIWA, ATANGAZA VITA KALI NA WAUZA UNGA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametangaza vita kali kwa watu wanaojihusisha na dawa za kulevya mkoani humo.
Akiongea leo jijini Dar es Salaam na viongozi wa serikali wa ngazi mbalimbali wa Mkoa huo, Makonda aliwataka viongozi wa ngazi za chini hususan Wenyeviti wa Mitaa kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Polisi kuwabaini watu wanaojishughulisha na dawa za kulevya.

Mkuu huyo wa Mkoa ameweka wazi kuwa hivi sasa haogopi kufa kwa kuwa tayari alimeshayafikia mafanikio aliyoyahitaji hivyo ni bora afe akipigania Taifa lake. Amewataka viongozi wenzake pia kutoogopa kufa kwakuwa lazima watakufa bali kinachoangaliwa ni sababu za kifo.

Amewataka wenyeviti wa mtaa ambao ndio wanaishi kwa karibu zaidi na wananchi waweze kuwasiliana moja kwa moja na wakuu wa wilaya pamoja na wakuu wa polisi kwa njia ya simu za mkononi ili kuwajulisha kuhusu vitendo vya kihalifu vinavyoendelea katika maeneo yao.

Katika kuhakikisha Jeshi la polisi linapata ari zaidi ya kufanya kazi ya kudhibiti uhalifu, Makonda amesisitiza kuwa atakuwa anatoa motisha ya shilingi milioni moja kwa polisi atakayeonekana kufanya vizuri zaidi.

“Polisi atakayefanya vizuri… mimi nitawapa shilingi milioni moja kila baada ya miezi mitatu kwa kuwashindanisha,” amesema Makonda.
at 2:32:00 PM
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

2 comments:

Anonymous said...

Sina uhakika na hili lakini wakati umefika wa kuwakamata na kuwachuchukulia hatua za kisheria tena kali hata wale wateja wanaotumia hayo madawa ya kulevya ili imfanye mtu anaeamua kuwa teja afikirie sana kabla ya kujiingiza katika upuuzi huo. Kwa nini sheria iwe kwa wale wauzaji wa madawa tu na kuwaacha wale wanaowashawishi kufanya hiyo biashara madawa wakisinzia mitaani tena wakati wa kazi? Nadhani katika kutangaza vita ya kweli basi mpaka mateja nao wakamatwe wapimwe na ikithibitika anatumia madawa ya kulevya afunguliwe mashitaka na si kufunguliwa mashitaka tu bali wao wawe ni moja ya chanzo cha uhakika cha kujua hayo madawa yanatoka kwa nani na isijali hilo teja ni mtu wa aina gani,awe super star hao ndio wawe wa kwanza kukamatwa kwa kuwa wao huwa na mvuto mkubwa katika jamii hasa vijana ambao wanawachukulia wao kama watu wa mfano katika maisha yao ya kila siku. Awe mtoto wa mkubwa au kigogo serikalini kamata tu sheria ni msumeno nadhani muheshimiwa Makonda ni kijana na utakuwa na weledi zaidi nnachokizungumza kwani wakati wa kulea maradhi umekwisha ni wakati wa kutibu sasa na kunako kutibu kama itatokezea mguu kukatwa ili kuzuia maradhi kutoenea mwili mzima basi hapana budi inabidi mguu ukatwe. Siku zote dawa haiwi kitu kitamu. Hata vyakula vingi vyenye siha zaidi kwa binaadamu ni vile vyakula vyenye ladha tata.kwa hivyo watanzania hatuna budi kuunga jitihada za muheshimiwa Makonda.

March 19, 2016 at 6:46 PM
Anonymous said...

asante mkuu, ila wakati haya madawa yanauzwa kwa wingi bado serikali iliyokuweka madarakani baada ya kuutafuta kwa kujinadi sana yalikuwa yanaendelea ilikuwa bora sana ungemueleza akaweka mkazo lakini nadhani ulikuw aunaogopa kwani ilikuwa sio serikali ya ukweli na uwazi.

Nirudie tena kusema asante na kwa maana umeona mkubwa wako wa kazi JPM msisitizo wa kazi na kuwajibikabila kuona aibu basi nadhani unaelewa maeneo yale muhimu hasa magomeni, masaki wilaya uliyoongoza ikiongoza kwa hayo madawa na wenye mtandao ni waliokuw wakubwa na hadi leo wakubwa zako hivyo jitahidi mdogo wangu labda utaweza kufanikiwa kwani wajanja nii wengi, ila usifanye pupa kwnai nao wanajua sana !!

March 19, 2016 at 10:49 PM

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

DJ Luke Joe

DJ Luke Joe

TANZANIA BLOGGERS' NETWORK

TANZANIA BLOGGERS' NETWORK

IskaJoJo Studios

IskaJoJo Studios

BEST MUSIC,BEST RATES

BEST MUSIC,BEST RATES
Music From The Past To The Present

RADIO YA UMOJA WA MATAIFA

RADIO YA UMOJA WA MATAIFA
TAARIFA YA HABARI & VYOMBO VYA HABARI

GENN RADIO

GENN RADIO
LISTEN LIVE

Clouds FM

Clouds FM
LISTEN LIVE

Radio Mbao

Radio Mbao
LISTEN LIVE

TONE ONLINE RADIO

TONE ONLINE RADIO
LISTEN LIVE

MJ RADIO

MJ RADIO
LISTERN ONLINE NOW

BONGO FLEVA

Tafuta

Kumbukumbu

Wadau

Tovuti na Blog Nyingine

  • 24 SEVEN 365
  • AL JAZEERA
  • BBC
  • BONGO CELEBRITY
  • BONGO STAR LINK
  • CHANGAMOTO YETU
  • CHEKA UPASUKE
  • CNN
  • DAILY NATION
  • DAILY NEWS
  • DINA MARIOS
  • DMK 411 BLOG
  • EBONY MAGAZINE
  • FACEBOOK
  • FIRST ROW SPORTS
  • FOX SOCCER
  • FULL SHANGWE
  • GENN MEDIA BLOG
  • GLOBAL PUBLISHERS
  • GSENGO BLOG
  • GUARDIAN UK
  • HABARI LEO
  • HAKI NGOWI
  • HIP HOP NEWS
  • IPP MEDIA
  • ISKAJOJO
  • JAMII BLOG
  • JIACHIE
  • K-VIS BLOG
  • KAHAWA TUNGU
  • KAMUSI
  • KITIME
  • KULIKONI
  • LADY JD
  • LILY MELODYY BLOG
  • LUNINGA
  • MAGANGA ONE
  • MAJIRA
  • MAMBOJAMBORADIO
  • MATUKIO
  • MAWASILIANO IKULU
  • MBEYA YETU
  • MICHUZI
  • MISS JESTINA GEORGE BLOG
  • MO BLOG
  • MOHAB MATUKIO
  • MTAA KWA MTAA BLOG
  • MWANANCHI
  • NAIROBI NEWS
  • NATION
  • NEW YORK TIMES
  • OTHMAN MAULID BLOG
  • PROFA
  • RAIA MWEMA
  • RED PEPPER
  • SAUTI TOKA NYIKANI
  • SHALUWA
  • SHAMIM
  • SPORT STAREHE
  • SPORTS SITE
  • STORM FM GEITA
  • SUBSONIC
  • SUFIANI MAFOTO
  • SUNDAY SHOMARI'S BLOG
  • SUPER SPORT
  • SWAHILI NA WASWAHILI
  • SWAHILI TV
  • SWAHILI VILLA
  • TAIFA JIPYA
  • TANZANIA BUSINESS DIRECTORY
  • TANZANIA DAIMA
  • TANZANIA GLAMOUR
  • TANZANIA HOTELS,WILDLIFE SAFARIS & CHEAP FLIGHTS
  • TAWICHITA
  • TEKNOHABARI
  • THA FUNK HOUSE
  • The Embassy of the United Republic of Tanzania in the United States
  • THE GLOBE AND MAIL
  • THE MONITOR
  • THE STANDARD
  • TMZ
  • TUNYFISH
  • TZMOMS
  • UHURU
  • UTNC
  • VOA-SWAHILI
  • WASHINGTON POST
  • WAVUTI
  • ZIMBIO

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

  • Diaspora marufuku kumiliki ardhi nchini Tanzania
    Tanzanians in the Diaspora continue to grapple with challenges that have seen most members either defrauded or lose confidence that th...
  • CESILIA FRANCIS AFANYA MNUSO WA KUJIPONGEZA
    Cesilia Francis akiingia ukumbini siku ya Ijumaa May 6, 2016 Clinton, Maryland Cesilia Francis akipata ukodak na mumewe. Cesilia...
  • UNITED STATES CONDEMNATION OF TANZANIA ELECTORAL PROCESS LACKS MORAL COMPASS.
    By Mohamed Matope Yesterday, the American Ambassador expressed great concern about the Tanzanian electoral process leading to the upcomi...
  • AMERICA AND THE GUN CULTURE
    BY MOHAMED MATOPE Last Monday America suffered the deadliest mass shooting in modern American history. A gunman rained down thou...
  • Je, unadhani nini hasa chanzo cha umaskini Tanzania?
    Tanzanite, Dhahabu, makaa ya mawe, almasi, urani, Mbuga za wanyama kama vile serengeti, Manyara, Ngorongoro, ardhi yenye rutuba, Mlima...
  • Charles Mihayo charged over death of two girls in Watsonia, Victoria
    Family photos of Indiana and Savana, who were killed at Watsonia. Charles Mihayo has been charged with two counts of murder. Pict...
  • Wanasheria naombeni msaada
    Nafikiri wote tumesikia na kusoma kwenye mitandao mbali mbali kuhusu ndoa ya Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr. Reginald  Mengi na former B...
  • MAGUFULI; REKODI YAKE YA UCHAPAKAZI INAIBEBA CCM
    Mhe. John Pombe Magufuli anayegombea kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa kwenye mkutano wa kampeni. Harakati za uchaguzi nchi...
  • MAPENZI NOMA DIAMOND ANASWA.AKIBEBESHWA POCHI NA ZARI
    Baada ya Diamond Platinumz a.k.a Chibu kunaswa na camera akiwa amembebea mkoba wa mpenzi wake Zarri Hussein, jiulize je wanaume wangapi t...
  • JK AMTAJA MUHUSIKA WA RICHMOND
    Rais Jakaya Kikwete amesema anashangazwa na Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu kumtaka amtaje mhusika wa Richmond wakati mwenye Richm...

LIVE TRAFFIC FEED

© 2015 Vijimambo - All Rights Reserved
Powered by Blogger.

HIT COUNTER BY GOOGLE