Advertisements

Wednesday, April 26, 2017

Mtatiro: CUF haina walinzi wa chama wenye bastola

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi, The Civic United Front (CUF) Julius Mtatiro amefunguka na kusema chama cha CUF hakina walinzi wa chama wenye bastola wala hakina walinzi wanaozunguka mitaani kufanya doria.

Julius Mtatiro ametoa ufafanuzi huo leo baada ya Mkurugenzi wa Habari CUF Taifa, ambaye anamuunga mkono Profes Ibrahim Lipumba  ndugu Abdul Kambaya kukiri kuwa ni kweli wao walituma vijana kwenda kwenye Kata ya Mabibo kufanya doria.

"Siku ambapo kikao kinafanyika Vinna Hotel, vijana wetu pia walikuwa kwenye doria, tulipozungumza na vyombo vya habari tulikiri na tunaendelea kukiri hatuna sababu ya kukataa kwamba tulituma vijana wetu na walikwenda kwenye doria" alisema Kambaya


Kufuatia taarifa hiyo ya Kambaya Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi, The Civic United Front (CUF) Julius Mtatiro amefunguka na kusema wao kama CUF hawana walinzi wa chama wenye bastola hivyo amelitaka jeshi la polisi limtumie huyu Kambaya kueleza kijana aliyekuwa na bastola yuko wapi na walikodishwa kutoka wapi.

"Leo amekiri kuwa lile Zombi lililopigwa na wananchi, Mabibo, eti lilitumwa na genge la Mungiki/Lipumba ili kufanya doria kwenye kata ya Mabibo. Yani eti Lipumba ana jeshi lake linalofanya doria na kupiga watu mitaani. Sasa Polisi wasitafute mchawi, huyu Abdul Kambaya aeleze lile zombi lililokuwa na bastola liko wapi na waliikodisha kutoka wapi? Alihoji Mtatiro

Mbali na hilo Mtatiro alizidi kusisitiza kuwa wao hawana walinzi wa chama

"Halafu, eti huyo msemaji wa Lipumba anasema "Zombi" hilo lililokamatwa ni "mlinzi wa chama". Napenda ifahamike kuwa CUF haina walinzi wa chama wenye bastola, na pia hakuna chama cha siasa chenye walinzi wanaozunguka mitaani kufanya doria, wameajiriwa na serikali ipi? Alihoji Mtatiro

No comments: