Advertisements

Saturday, May 26, 2018

Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji waendelea jijini Arusha

Bw.Benard Haule Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji na

Sekta za Uzalishaji, akizungumza kwenye mkutano wa Baraza la
Kisekta

 la Mawaziri wa  Biashara, Viwanda,Fedha na Uwekezaji 
unaoendelea kufanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo katika

majengo ya ofisi za Makao Makuu
 ya Jumuiya ya Afrika 

Mashariki



jijini 


Arusha.

     
Mkutano wa Kisekta wa Baraza la Mawaziri wa Biashara,Viwanda, Fedha na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaendelea kufanyika jijini Arusha. Mkutano huu unafanyika kwa kipindi cha siku saba (7) kuanzia tarehe 25 hadi 30 Mei, 2018. Pamoja na mambo mengine yatakayojili, Mkutano huu unatarajia kufanya yafuatayo:-
  • Kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa maagizo  na maamuzi yaliyofanywa na mkutano uliopita wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji;
  • Kupokea na kajadili taarifa ya majadiliano ya awali ya bajeti ya Baraza la Mawaziri wa Fedha la Jumuiya ya Afrika Mashariki;
  • Kupokea na kujadili taarifa ya Kamati ya Forodha
  • Kupokea na kujadili taarifa ya Kamati ya Kisekta ya Biashara;
  • Kupokea na kujadili taarifa ya Kamati ya Mamlaka ya Ushindani;
  • Kupokea na kujadili taarifa ya Kamati ya Viwango ya Jumuiya ya Afrika Mashariki; na
  • Kupokea na kujadili taarifa kutoka Kamati ya Kisekta ya Viwanda.

Mkutano huu anafanyika katika ngazi tatu ambazo ni ngazi ya waalam, ngazi Makatibu Wakuu, na ngazi ya Mawaziri.

Mkutano huu umehudhuriwa na wajumbe kutoka nchi zote  wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki. 


Bw. Benard Haule Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji akichangia wakati wa Mkutano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda,Fedha na Uwekezaji unaondelea jijini Arusha. 

Bw. Raymond Agaba Kamishna wa Biashara za Ndani (kushoto) kutoka Jamhuri ya Uganda akiongoza mkutano. Kulia ni Bibi Flavia Busingye Afisa Mkuu wa Forodha,ufuatiliaji na utekelezaji kutoka Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki

Mkutano ukiendelea

No comments: