Advertisements

Friday, July 20, 2018

MABALOZI WANNE WAAGWA JIJINI DAR ES SALAAM

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) aliyesimama katikakti akiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Mabalozi waliomaliza muda wao wa uwakilishi nchiniTanzania. Mabalozi hao, wakwanza kutoka kushoto ni Balozi wa Norway, Mhe. Hanne-Marie Kaarstad, Balozi wa Malawi, Mhe. Hawa Olga Ndilowe, Balozi wa Sweden, Mhe. Katarina Rangnitt na Balozi wa Canada, Mhe. Ian Myles. Mhe. Dkt. Mahiga aliandaa hafla ya kuwaaga Mabalozi hao iliyofanyika jijini Dar Es Salaam tarehe 17 July 2018. Katika hafla hiyo, Dkt. Mahiga aliwashukuru Mababalozi hao kwa niaba ya Serikali zao kwa mchango mkubwa wanaotoa kuboresha sekta mbali mbali hapa nchni zikiwemo za Elimu, Afya, Biashara, Kilimo pamoja na Miundombinu. Aidha, Mabalozi pia walipata nafasi ya kutoa neno la shukrani kwa Wizara pamoja na watumishi wake kwa ujumla kwa kuwapa ushirikiano wa kutosha uliowawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi hapa nchini. 
Dkt. Mahiga akizungumza kwenye hafla ya kuwaaga Waheshimiwa Mabalozi walio maliza muda wao wa uwawakilishi nchini. 
Sehemu ya Mabalozi walio hudhuria hafla hiyo wakisimsikiliza kwa makini Mhe. Dkt. Mahiga (hayupo pichani). 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya naAmerika, Bw. Jestas Nyamanga (kulia) pamoja na Balozi Rangnitt nao wakimsikiliza kwa makini Dkt. Mahiga. 
Sehemu nyingine ya Mabalozi waliohudhuria hafla hiyo 
Mabalozi walio maliza muda wa uwakilishi nchini wakigonga glasi na Waziri Mahiga ikiwa ni ishara ya kuwatakia Viongozi wa Nchi zao Afya njema na Baraka tele kwenye kufanikisha gurudumu la maendeleo. 
Dkt. Mahiga akimkabidhi Balozi wa Sweden picha ya mchoro wa Tembo wa Tatu pamoja na Mlima Kilimanjaro ikiwa ni sehemu ya kuendelea kuikumbuka Tanzania pamoja na kuendelea kuvitangaza vivutio vinavyopatikana nchini. 
Balozi wa Malawi naye alipewa Picha yenye tembo wa Tatu na mlima Kilimanjaro 
Dkt. Mahiga akimkabidhi Balozi wa Norway picha inayofanana na wenzake isipokuwa yake ilikuwa na Michoro ya Wanyama aina ya Twiga, Tembo pamoja na Mlima Kilimanjaro. 
Balozi wa Canada naye alipata zawadi ya picha yenye mchoro wa Tembo pamoja na Mlima Kilimanjaro, kwa pamoja Mabalozi hao walionyesha kuzifurahia zawadi hizo. 
Dkt. Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi waliomaliza muda wa uwakilishi nchini pamoja na Mabalozi ambao bado wanaendelea kuziwakilisha nchi zao. 

No comments: