Advertisements

Wednesday, August 1, 2018

WAZIRI LUGOLA, WADAU WA USAFIRI NA USAFIRISHAJI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati), akizungumza na wadau wa usafiri na usafirishaji nchini katika kikao cha kujadili jinsi ya kupambana na ajali za barabarani. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam. Kushoto kwa Waziri ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu, akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima. Kulia ni Naibu Waziri wa Kazi, Vijana, na Ajira, Antony Mavunde. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati), akimsikiliza Naibu Waziri wa Kazi, Vijana, na Ajira, Mhe Antony Mavunde, alipokua akiwafafanulia jambo wadau wa usafiri na usafirishaji kuhusu jinsi ya kupambana na ajali nchini. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto kwa Waziri Lugola ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu, akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akifafanua jambo kwa wadau wa Usafiri na Usafirishaji jinsi ya kupambana na ajali za mara kwa mara nchi. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Ndani jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Waziri Kangi Lugola wa wizara hiyo akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw Kailima Ramadhani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akimsikiliza Omari Mponda, Kaimu Rais Chama cha Wasafirishaji Tanzania akichangia jambo jinsi wadau hao wanavvyoweza kushirikiana na wizara hiyo katika kupambana na ajali za barabarani .. Kushoto kwa Waziri ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu, akifuatiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Ramadhani Kailima. Kulia ni Naibu Waziri wa Kazi, Vijana, na Ajira, Antony Mavunde. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Ndani jijini Dar es Salaam

No comments: