ANGALIA LIVE NEWS

Showing posts with label Matukio. Show all posts
Showing posts with label Matukio. Show all posts

Monday, November 18, 2024

STANDARD CHARTERED YAPANDA MITI 2000 KIGONGONI BAGAMOYO



Benki ya Standard Chartered imepanda miti 2000 ya matunda na kivuli katika Shule ya Msingi Kigongoni iliyopo kata ya Magomeni Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani ikiwa ni mwendelezo wa kampeni waliyoianzisha miaka mitatu iliyopita kuunga mkono juhudi za serikali za utunzaji mazingira.

Akizungumza shuleni hapo Ofisa Mkuu Mwendeshaji na mambo ya Teknolojia wa benki hiyo Christopher Vuhahula aliwahimiza wanafunzi wa shule hiyo na uongozi kuitunza na kuahidi kuifutilia kuona asilimia ngapi imeweza kuendelea na kukua.

Alisema tangu wameanza kampeni ya upandaji miti wameshapanda jumla ya miti 6500 na kwa upande wa Bagamoyo tayari wameshapanda katika shule tano na kuahidi kuendelea kupanda miti ili nchi iwe mahali pazuri katika eneo la mazingira.

"Tunapokuja kwa wanafunzi wanajifunza wao na ni elimu, tukihamasisha kwa kupanda wakiwa wanaona baba zao, kaka zao, dada zao na Shangazi zao wanavyofanya kutunza mazingira wanajifunza wakiwa wadogo wanamwagilia aliye darasa la kwanza akimwagilia mpaka amalize darasa la saba na kuona matokeo ya ule mti atafurahia na kuchukua elimu kwa vitendo na kupeleka nyumbani," alisema.

Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga aliwashukuru Standard Chartered kwa kushiriki kutoa miche hiyo na kuhimiza taasisi nyingine kuiga mazuri huku akiwataka viongozi wa halmashauri ya Bagamoyo kuweka mkakati kuhakikisha miti inayopandwa inaishi.

Alisema kampeni hiyo ili iweze kufanikiwa lazima kila mmoja ashiriki kwa maana ya wananchi, taasisi mbalimbalina kwamba wanafanya juhudi za kupanda miti kwasababu ndio njia sahihi iliyothibitika na ya uhakika ya kupambana na hewa ukaa, pia ndio maisha ya viumbe hai wanaotumia miti kuvuta hewa ya oksijeni na kabonidayoksaidi.

'Miaka 10 iliyopita kuna maeneo ya Bagamoyo yalikuwa Msitu , kuna maeneo yamevunwa sana kuliko juhudi za kupanda na kuhihifadhi hivyo, tusipopanda miti hii kutakuwa Jangwa

Tuendelee kupanda bila kuchoka na ni lazima juhudi za kupanda zizidi nguvu tuliyotumia katika kuharibu,"alisema.

Ndemanga alisema kuna watu wanachimba mchanga wanaharibu mazingira na kuagiza Halmashauri ya Bagamoyo kuhakikisha wanapotoa vibali vya watu kuchimba waingie nao mkataba kwamba wakishamaliza wafukie mashimo vinginevyo kunaweza kuchangia mabwawa yasiyokuwa na faida na ni hatari kwa watoto wanaocheza maeneo hayo.

Awali, Head of Public Sector and Financial Institution wa Standard Chartered Sapientia Balele alisema ni muhimu kulinda mazingira kwa vizazi vya sasa na vijavyo kulinda mabadiliko ya tabia nchi na kuahidi kuendelea kushirikiana na serikali kusapoti miradi mbalimbali kuendelea kulinda mazingira.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Shauri Selanda alisema katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi benki hiyo imepanda miti takribani 4500 katika shule mbalimbali za msingi kwenye Halmashauri hiyo.

Alisema Tatedo kwa kushirikiana na Halmashauri hiyo nao watapanda miti 2000 hivyo jumla itakuwa 4000 akisema shule ya Kigongoni itakuwa na mazingira mazuri ya kujisomea.
Mkuu wa Wilaya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga, akipanda mti katika Kampeni ya upandaji miti iliyotolewa na benki ta Standard Chartered katika Shule ya Msingi Kigongoni iliyopo wilayani humo mkoani Pwani.
Mkuu wa Wilaya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga (kushoto), Mkuu wa Uwendeshaji na mambo ya Teknorojia wa benki ya Standard Chartered, Christopher Vuhahula (kulia), wakiwakabidhi miti ya matunda nay a kivuli wanafunzi wa Shule ya Msingi Kigongoni iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani wakati wa upandaji miti iliyotolewa na benki hiyo shuleni hapo.


Mkuu wa Uwendeshaji na mambo ya Teknorojia wa benki ya Standard Chartered, Christopher Vuhahula (katikati), akipanda mti na wanafunzi wa Shule ya Msingi Kigongoni iliyopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani kufuatia kampeni ya benki hiyo ya kupanda miti katika Mkoa huo ili kutunza mazingira kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mary Musa.
Wafanyakazi wa Benki ya Standard Chartered, wakipanda miti katika eneo la Shule ya Msingi Kigongoni, iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani kufuatia Kampeni ya benki hiyo ya kupanda miti ili kutunza mazingira mkoani humo.

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kigongoni, iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani, wakishirikiana na wafanyakazi wa benki ya Standard Chartered, kupanda miti katika eneo la shule hiyo katika Kampeni ya benki ya kupanda miti ili kutunza mazingira mkoani humo.








Sunday, January 7, 2024

MAHUNDI ATOA SIKU SABA MENEJA RUWASA LUSHOTO KUKAMILISHA ULAZAJI WA MABOMBA .

NAIBU Waziri wa Maji  Mhe.Mhandisi Maryprisca  Mahundi (Mb) amemuagiza Meneja wa Ruwasa wa Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga Mhandisi Erwin Sizinga aweze kuhakikisha wanakamilisha ulazaji wa bomba wa umbali wa kilomita 2.8 ndani ya wiki moja ili wananchi wa Kata ya  Ubiri na Ngulwi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.


Kadhalika  Mhandisi Mahundi amemuagiza Mkandarasi anayejenga Mradi wa Maji wa Magamba ahakikishe anaongeza kasi ya utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ili aweze kukamilisha kwa wakati.

Mhandisi Mahundi ametoa maagizo hayo leo Januari 6  2024, alipotembelea na kukagua utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maji ya Magamba na Mradi ya Maji Irente-Yoghoi-Ngulwi iliyopo Wilayani Lushoto Mkoani Tanga.

"Ili wananchi  elfu 30,835 wa maeneo ya Magamba, Kwesimu, Bara, Jegestal, Kambi namba nne, Chakechake, Kitivo, Maguzoni, Sinza, Lushoto Mjini, Mabwawani, Kipembe na Kialilo waweze kupata huduma ya maji miradi hii inapaswa kukamilika kwa wakati"amesema Mhandisi Mahundi

Naye  Mbunge wa Jimbo la Lushoto, Mhe. Shaban Shekilindi ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutekeleza miradi ya maji kwenye jimbo hilo huku akisema  wananchi wengi watapata huduma ya maji huku akiwasisitiza wakandarasi kukamilisha kwa wakati.




Friday, November 10, 2023

WATEJA WA Y9 MICROFINANCE KUONGEZEWA DAU LA MKOPO SASA WAWEZA KUKOPA HADI LAKI TATU

 

 Na Mwandishi wetu.


Dar es Salaam. Taasisi ya kifedha ya Y9 Microfinance imeendelea na utaratibu wake wa kukabidhi zawadi kila wiki ambapo wiki hii wamekabidhi zawadi ya pikipiki mbili kwa washindi wa Droo ya nne kwa wakazi wa Njombe na Songea.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo Mkurugenzi wa Mauzo na Usambazaji wa Taasisi ya Y9 Microfinance Bw. Fredrick Mtui amesema kuwa taasisi ya Y9 ilianzishwa mahususi kuwasadia na kuinua mitaji ya wale wenye kipato cha chini na watanzania wote nchini.

Lengo kuu la Y9 Microfinance ni kuhakikisha kila mtanzania anapata fursa hii kwa kuhakikisha anapakua app ya Y9 Microfinance na kupata huduma ya tatu ambazo ni mkopo wa fedha taslimu.

Kwa upande wake Meneja Masoko wa Taasisi ya Y9 Microfinance, Sophia Mang’enya ambaye pia alieleza kuwa hii ni fursa kubwa sana kwa watanzania kwani Taasisi ya Y9 umeongeza pia kiwango cha mkopo pia siku za kulipa deni la mkopo

Mang’enya ameeleza kuwa jwasasa mteja wa Y9 anaweza kukopa kuanzia elfu mbili hadi laki tatu na muda wa kurejesha ni siku 9 ambapo awali kiwango cha juu kilikuwa laki moja na muda wa kurejesha ni siku tatu

Ameeleza kuwa nia na madhumuni ya kuongeza kiwango cha mkopo nikuridhishwa na mwenendo mzuri wa ulipaji kwa wateja wao hivyo amewasihi watanzania wachangamkie fursa hii ambayo haina mashart magumu.

amewapongeza washindi wote kwa kujiunga na huduma zao na kuweza kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo simu, pikipiki vilevile ameongeza kwamba kwenye droo ya mwisho ambayo itanyika katikati ya mwezi Disemba kutakuwa na zawadi kubwa zaidi ya gari aina ya Toyota IST. na zawadi nyengine kemkem

Alisema kuwa washindi hao wameshinda zawadi hizo baada ya kupakuwa App yetu na kukopa kupitia app na kurejesha mikopo yao ndani ya muda uliowekwa kwa mujibu wa taratibu zetu.

Alisema kuwa zawadi bado zipo nyingi kikubwa Watanzania kuendelea kutumia humu zetu ili kujishindia zawadi.

Leo pia tumechezesha droo ambapo tumepata washindi wawili ambao ni Riziki Makame ambae amejishindia pikipiki ya matairi mawili pamoja na mkazi wa Arusha Bw. Peter ambae amejishindia simu janja.




Friday, November 3, 2023

WASHINDI SHINDANO LA BE ROAD SAFE KWA NJIA YA SANAA WATUNUKIWA TUZO, RC DAR AIPONGEZA PUMA ENERGY TANZANIA

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Amend wametoa tuzo kwa wanafunzi ambao wameibuka washindi wa michoro ya usalama barabarani kupitia  kampeni ya Be Road Safe kwa njia ya sanaa.

Katika utoaji wa tuzo huo umefanyika katika Shule ya Msingi Kibugumo iliyopo Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila ambaye aliwakilishwa ba Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Halima Bulembo .

Kampeni hiyo inalenga kuleta mageuzi ya usalama wa watoto na vijana barabarani nchini Tanzania huku ikielezwa wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Kubugumo,  Kufaru,  Msewe, Kibasila na Mtambani wameshiriki katika kampeni hiyo kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo shindano la kuchora.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila,  wakati wa utoaji tuzo hizo kwa washindi,  Mkuu wa Wilaya Halima Bulembo amesema wanaipongeza kampuni ya Puma Energy Tanzania pamoja na Ammend kwa kutoa elimu ya usalama barabarani kwa watoto walioko shule za msingi.

Asema mafunzo ya usalama barabarani kwa watoto walioko katika shule za msingi yatasaidia kupunguza ajali za barabarani hususan katika maeneo ambayo mafunzo hayo yametolewa huku akishauri elimu hiyo yatolewe nchi nzima kuongeza uelewa.

Amesisitiza Serikali inaamini kwa kufanya hivyo kitaokolewa kizazi cha sasa na kijqacho kwa kuwa elimu ya matumizi bora ya barabara inaendelea kusambaa.

Amesema kuwa kupitia mafunzo ya usalama barabarani kwa watoto hususan walioko katika shule za msingi Puma imefanya jambo kubwa katika kuepusha ajali za barabarani ambazo zimekuwa sikiisababishia nchi hasara kubwa kwa kupoteza nguvu kazi na mali.

"Mafunzo ya elimu ya usalama barabarani yaliyotolewa na Puma Energy Tanzania kwa kushirikiana na Ammend katika shule tano ni vyema yakatolewa pia katika shule nyingi zaidi kuwajengea uwelewa watoto wangi wa Dar es Salaam na hata nje ya mkoa huo.

"Serikali ya mkoa (Dar es Salaam) tunaamini kuwa kwa kufanya hivi tunaokoa kizazi cha sasa na kijacho kwa kuwa elimu ya matumizi bora na sahihi ya barabarani inaendelea kusambaa," amesema Bulembo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Fatma Abdallah, amesema mafunzo yaliyotolewa kwa wanafunzi hao ni utekelezaji wa mpango wa 'Be road safe Africa) unaotekelezwa na Ammend katika nchi tano za Afrika ambazo ni Zambia, Zimbabwe, Tanzania, Botswana na Ghana.

Amesema kuwanzishwa kwa mpango huo kunatokana na takwimu mbaya za ajali za barabarani ambazo zinasababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali.

"Nchini Tanzania pekee Jeshi la Polisi kupitia kikosi cha Usalama Barabarani kimetoa takwimu zinazoonyesha kutokea kwa vifo 1,545 na majeruhi 2,278 kwa mwaka 20222 kutokana na ajali 1,720 za barabarani.

Fatma akizungumzia kampeni hiyo ya 'Be Road Safe' amesema kuwa ni jukwaa muhimu shirikishi linalokuza jamii salama kwa watoto.

 "Kupitia mashindano hayo ya kuchora tumeongeza ubunifu na uelewa thabiti wa kanuni za usalama barabarani miongoni mwa wanafunzi na kuongeza ufahamu kwa jamii ya Watanzania.

Amesema tangu kuanzishwa kwa mpango huo mwaka 2013 'Be Road Safe' umekuwa mwanga wa matumaini na kwamba ni msingi wa kimkakati wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) wa kampuni hiyo chini ya mpango mkuu wa 'Be Puma Safe' ambao pia unajumuisha uwezeshaji wa wananchi hususan vijana.

Hafla hiyo iliyofanyika Shule ya Msingi Kibugumo ilihidhuriwa na wadau mbalimbali akiwemo Mkuu wa Dawati la Elimu ya Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi wa Polisi Michael Deleli, Mkurugenzi wa Shirika la Ammend Simon Kalolo, walimu na wanafunzi kutoka shule zilizoshiriki mafunzo na shindano hilo.

 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Halima Bulembo(wa tatu kulia) akimkabidhi kikombe mwanafunzi wa darasa sita katika Shule ya Msingi Kibugumo Feisali Msiakwe baada ya kuibuka mshindi wa mchoro wa usalama barabarani na kuifanya shule yake kuwa kinara katika mashindano hayo yaliyoandaliwa na Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Amend.Wengine katika picha hiyo ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Fatma Abdallah( wa kwanza kushoto), Kaimu Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kibugumo Salvatory Lasway ( wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo( wa kwanza kulia).

Mwanafunzi wa darasa sita katika Shule ya Msingi Kibugumo Feisali Msiakwe akinyanyua juu kikombe cha ushindi baada ya mchoro wake wa kuelimisha kuhusu usalama barabarani kushinda katika shindano la michoro ya usalama barabarani kwa Mkoa wa Dar es Salaam.Feisali amepata kitita cha Sh.500, 000 na shule yake baada ya kuibuka mshindi wa mchoro wa usalama barabarani na kuifanya shule yake imepata Sh.milioni tano ambazo zimetolewa na Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania kupitia Mkurugenzi wake Fatma Abdallah(wa kwanza kushoto waliosimama.)



Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Halima Bulembo(wa tatu kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Fatma Abdallah( wa kwanza kushoto) wakiwa wameshika mfano wa hundi ya Sh.milioni tano iliyotolewa kwa Shule ya Msingi Kibugumo baada ya mwanafunzi wake Feisali Msiakwe ( wa nne kushoto) kuibuka mshindi wa mashindano ya mchoro wa usalama barabarani katika mkoa wa Dar es Salaam.Mashindano hayo yameandaliwa na Puma kwa kushirikiana na Shirika la Amend Tanzania.Wengine katika picha hiyo ni walimu na wadau wa usalama barabarani.













Monday, January 2, 2023

MSIMU MPYA KAMPENI YA MAMA NIVISHE VIATU YA SAMIA SULUHU KUANZA TENA BARA, ZANZIBAR

  

Na Mwandishi Wetu 

MSIMU mpya wa Kampeni ya Samia Nivishe Viatu inayofanywa na Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao inatarajia kuanza kutekelezwa katika mikoa ya Lindi,Mtwara,Songea, Iringa pamoja na Visiwani Zanzibar.

Hadi sasa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao chini ya Uongozi mahiri wa Mwenyekiti wake Steven Mengele maarufu kwa jina la Steve Nyerere imeshawavisha wanafunzi wengi viatu kupitia Kampeni ya Samia Nivishe Kiatu 2022 na sasa msimu mpya wa kampeni utaendelea kwenye mikoa hiyo.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao Steve Nyerere amesema kwamba  lengo la kampeni hiyo ni kuhakikisha kila mtoto mwanafunzi mwenye uhitaji anavaa Kiatu cha Samia Suluhu.

"Msimu mpya unaanza Samia nivishe kiatu  utafanyika katika Mkoa wa Lindi, Mtwara,Songea Iringa pamoja na Visiwani Zanzibari, kote huko tunataka wanafunzi wavae kiatu cha Samia Suluhu.

"Kiatu cha Samia Suluhu kitavaliwa katika shule mbalimbali nchini na tutapita kwenye shule na kuwakabidhi  watoto wenyewe viatu hivyo kwa ajili ya mazingira mazuri ya masomo kwa watoto,"amesema Stive Nyerere alipokuwa akielezea kuanza kwa msimu huo mpya.

Kwa mujibu wa Steve Nyerere Kampeni ya Nivishe Viatu Ya Samia Suluhu itafanyika nchi nzima na kwa sasa wameshapita katika mikoa kadhaa kwa kuanza na Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani na baadae Mkoa wa Tabora.

Aidha ametumia nafasi hiyo kuelezea kubwa tangu kuanza kwa Kampeni hiyo wanashukuru kwa kuungwa mkono na wadau mbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine wameifanya Kampeni hiyo kuwa rahisi kwao huku akisisitiza wataendelea nayo hadi wahakikishe wanafunzi wenye uhitaji wa viatu kote nchini wanafikiwa na kuvaa Kiatu cha Samia Suluhu.

Kampeni hiyo ilizinduliwa mwaka 2022 na Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao ambayo inaundwa na wasanii wa filamu na muziki Tanzania na kauli mbiu yake ni 'Samia Nivishe viatu 2022' huku dhumuni kuu likiwa kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kwenye sekta ya elimu.







Tuesday, December 27, 2022

Msanii "DK Regani" anakukaribisha kuskiliza wimbo wake mpya Emi lo kna


 Msanii wa muziki kutoka Nigeria, DK Regan ana kukalibisha  kuskia wimbo wake mpya m ‘Emi lo kan’ wimbo umefanya na prodyuza  Jaysynths na anakualika uitazame kwa kubofya link hapa chini;

Saturday, November 26, 2022

NSSF ILIVYOSHIRIKI KATIKA MAONESHO YA WIKI YA HUDUMA YA FEDHA KITAIFA JIJINI MWANZA

 

 


Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) ulishiriki katika maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha Kitaifa katika viwanja vya Rock City Jijini Mwanza.


NSSF ilitumia maonesho maonesho hayo kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi, matumizi ya mifumo ya TEHAMA kwa mwanachama na mwajiri ili kumrahisishia huduma bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF, kusikiliza na kutatua kero za wanachama na kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji ikiwemo miradi ya nyumba za kisasa, miradi ya uwekezaji ya majengo ya Mzizima Tower na Mwanza pamoja na viwanja.
Meneja wa NSSF Mkoa wa Mwanza Emmanuel Kahensa akitoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa wanafunzi wa Chuo cha Utalii Mwanza waliofika katika banda la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha jijini Mwanza.

Mkurugenzi wa Hifadhi ya Jamii kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Festo Fute (wa pili kulia), Meneja wa NSSF Mkoa wa Mwanza, Emmanuel Kahensa (wa kwanza kulia), Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Hifadhi ya Jamii, Omary Mziya (wa kwanza kushoto) na Afisa Utawala Mkuu wa NSSF Mkoa wa Mwanza, Flora Ndutta (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya viongozi hao kutembelea Banda la NSSF wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha jijini Mwanza.








Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Hassan Chande, (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Afisa Utawala Mkuu wa NSSF Mkoa wa Mwanza, Flora Ndutta (kulia), kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Mfuko katika banda la NSSF wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha jijini Mwanza.

Afisa Utawala Mkuu wa NSSF Mkoa wa Mwanza Flora Ndutta (kushoto), akitoa huduma kwa wananchi waliofika katika banda la Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakati wa Maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha jijini Mwanza. (wa pili kushoto) ni, Mhasibu wa NSSF Mkoa wa Mwanza, Said Othman Mfuru.

Afisa TEHAMA wa NSSF, Janeth Bwire, akitoa maelezo kwa mwanachama jinsi ya kujihudumia kupitia simu yake kupitia mfumo wa WhatsApp chatbot. Huduma hiyo inapatikana kwa njia ya Whatsapp ambapo mwanachama halazimiki kufika Ofisi katika ofisi za NSSF. Elimu hiyo ya jinsi ya kutumia mifumo inatolewa katika banda la NSSF kwenye Maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha jijini Mwanza.

Afisa Matekelezo Mwandamizi, sekta isiyo rasmi Diagi Janguo akimwandikisha Mwanachama mpya wa NSSF alipotembelea banda la NSSF kwenye Maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha jijini Mwanza

Afisa Usalama Mwandamizi wa NSSF,Mfaume Kambangwa akitoa elimu kwa wanachama wa NSSF waliotembelea banda la NSSF namna Mfuko unavyopinga vitendo vya rushwa na kuwa huduma zote zinatolewa bure. Elimu hiyo ya kupinga rushwa katika maeneo ya kazi inatolewa katika Maonesho ya Wiki ya Huduma ya Fedha jijini Mwanza

Friday, November 25, 2022

Benki ya Standard Chartered yashirikiana na SheFound kuelimisha wanawake kuhusu usalama wa mitandaoni (cyber security)

 

 
Benki ya Standard Chartered kwa kushirikiana na SheFound wamewakutanisha wanawake zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kujadili changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.

Wafanyabiashara hao wanawake wamekutanishwa Novemba 23,2022 jijin Dar es es salaam,ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered, Herman Kasekende aliwakilishwa na Jerry Agyeman-Boateng.

Akitoa maoni yake kwa niaba ya Benki, Jerry Agyeman-Boateng ambaye ni Mkuu wa Biashara Wateja Wakubwa, wa Kati na Taasisi za Fedha amesema lengo lao ni kuendesha biashara na ustawi kupitia utofauti wao wa kipekee.

Aidha amesema katika enzi ya kisasa ya kidijitali, wahalifu wa mtandao wanazidi kulenga mashirika mengi. Shirika lolote linaweza kulengwa na wahalifu wa mtandao iwapo hawatadhibitiwa ipasavyo .Tuna jukumu la kutekeleza ili kuhakikisha tunafahamishwa vyema kuhusu mashambulizi ya mtandaoni yanayoweza kutokea ili tunapofanya biashara tuwe salama."

Hivyo amesema benki hiyo inaishukuru SheFound kwa kushirikiana nayo kwenye kuwajengea uelewa wanawake kuhusu masuala ya usalama kwenye mitandao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa SheFound Vannesa Kisowile pamoja na mambo mengine ameeleza kwamba zaidi ya asilimia 60 ya mandhari ya MSME barani Afrika yanaundwa na wanawake wajasiriamali kwa kutumia teknolojia.

Amesema ni muhimu kuongeza ufahamu kuhusu mambo ya usalama wa mtandao ili kupunguza matukio ya wizi yanayofanyika mtandaoni."Hii itasababisha ukuaji na uendelevu wa biasharapamoja na maendeleo ya jumla ya kijamii na kiuchumi."

Pia kulikuwa na mjadala ulihusisha wadau wengine wakiwemo wabobezi kwenye mambo ya biashara na tehama ambao walishiriki kutoa elimu na kubadilishana ujuzi na maarifa na wafanyabiashara hao.

Akizungumzia dhamira ya Benki ya kusaidia wanaoanza biashara, Busara Raymond ambaye ni Meneja wa Bidhaa za Fedha katika Benki ya Standard Chartered amesema Benki imewezesha kusaidia uanzishaji wa biashara kupitia SC Ventures ambacho ni kitengo cha biashara kinachohusika kuchochea na kukuza uvumbuzi. Pia kuwekeza kwenye teknolojia ya kifedha na kuchunguza mifumo mbadala ya biashara. SC Ventures iko wazi kwa biashara zote zinazoanzishwa ambazo zina maoni ya kibiashara yanayofaa.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama Tanzania, Dkt Nkundwe Mwasaga akizungumza kwenye moja ya kongamano lililoandaliwa na Benki ya Standard Chartered kwa kushirikiana na taasisi ya SheFound ambapo liliwakutanisha wanawake zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kujadili changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.



Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama Tanzania, Dkt Nkundwe Mwasaga (wa tatu kulia) akizungumza kwenye moja ya kongamano lililoandaliwa na Benki ya Standard Chartered kwa kushirikiana na SheFound ambapo liliwakutanisha wanawake zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kujadili changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.
Mtaalamu wa masuala ya 'IT' na Mhamasishaji wa Jamii kuhusu masuala ya Kifedha kutoka Benki ya Standard Chartered Bupe Mwakabaga akieleza jambo kwenye kongamano hilo lililoandaliwa na Benki ya Standard Chartered kwa kushirikiana na taasisi ya SheFound ambapo liliwakutanisha wanawake zaidi ya 40 ambao ni wafanyabiashara mbalimbali kwa ajili ya kujadili changamoto na fursa katika nafasi ya usalama kwenye mitandao.Pichani kushoto ni MKurugenzi wa Kampuni ya ya Meriitech Esther Mwasaga


Baadhi ya washiriki wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye kongamano hilo