Sunday, February 14, 2010

Haiti kuomboleza leo


pichani mama wa Haiti amefunikwa na kifusi jan 12,2010 mji wa Port-Au-Prince baada ya tetemeko kubwa lililoikumba nchi hiyo
Watu wa Haiti wametenga leo kama siku kuu ya kitaifa ya kuomboleza maelfu ya watu waliofariki katika tetemeko la ardhi lililotokea mwezi mmoja uliopita.
Ibada inatarajiwa kufanywa katikati mwa mji wa Port-au-Prince, ambako Ikulu ya Rais inaonekana ikiwa imeporomoka, kama mijengo mingine kote mjini. Serikali imepanga kuweka televisheni kubwa sehemu mbalimbali za mji ili watu wafuatilie kikamilifu ibada hiyo.
Tetemeko hilo lilisababisha vifo vya zaidi ya watu 230,000 na kuwaacha wengine zaidi ya milioni moja bila makaazi.

No comments: