Thursday, August 20, 2015

WASANII KUIPIGIA DEBE CCM NA TAMASHA LA MAMA ONGEA NA MWANAO 2015

Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kutoka kulia ni Wellu Sengo (Matilda). Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kutoka kulia ni Wellu Sengo (Matilda).Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kulia ni Yobnesh Yusuph (Batuli) na kushoto ni Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere wakiwa katika mkutano huo. Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kulia ni Yobnesh Yusuph (Batuli) na kushoto ni Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere wakiwa katika mkutano huo.
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mratibu wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere akizungumza na waandishi wa habari leo juu ya tamasha hilo. Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mratibu wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere akizungumza na waandishi wa habari leo juu ya tamasha hilo.Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu (kulia) akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kutoka kulia ni Wellu Sengo (Matilda) na Yobnesh Yusuph (Batuli). Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu (kulia) akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kutoka kulia ni Wellu Sengo (Matilda) na Yobnesh Yusuph (Batuli).Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kulia ni Yobnesh Yusuph (Batuli) na kushoto ni Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere wakiwa katika mkutano huo. Mwenyekiti Msaidizi wa Tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM, Wema Sepetu akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam juu ya tamasha na kampeni zao. Kulia ni Yobnesh Yusuph (Batuli) na kushoto ni Steve Mengele a.k.a Steve Nyerere wakiwa katika mkutano huo.Baadhi ya wasanii na makada wa CCM ambao watajumuika katika tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano na waandishi wa habari. Baadhi ya wasanii na makada wa CCM ambao watajumuika katika tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015 litakaloipigia kampeni CCM wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano na waandishi wa habari.Baadhi wa aandishi wa habari wakiwasikiliza wasanii hao na waratibu wa tamasha  la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015. Baadhi wa aandishi wa habari wakiwasikiliza wasanii hao na waratibu wa tamasha la MAMA ONGEA NA MWANAO 2015.

 WASANII ambao ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameandaa Tamasha kubwa kuzunguka nchi nzima kwa pamoja na kukinadi chama hicho tawala pamoja na Sera zake ili kiweze kushinda Uchaguzi Mkuu onaotarajia kufanyika Oktoba Mwaka huu (2015).

 Tamasha hilo litakalojulikana kama "MAMA ONGEA NA MWANAO 2015" limeandaliwa na baadhi ya wasanii makada wa CCM wapatao 250 ambao watazunguka mikoa zaidi ya 10 kukipigia kampeni chama hicho tawala ili kiweze kupewa ridhaa tena na Wananchi ya kuendelea kuongoza nchi. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari Mwenyekiti Msaidizi wa tamasha hilo, Wema Sepetu alisema madhumuni ya tamasha la Mama Ongea na Mwanao 2015 ni kulinda mazuri yote yalioasisiwa na CCM kupitia viongozi wake akiwemo Baba wa Taifa Mwalimu Julias Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume. Msanii Sepetu akiyataja masuala hayo yalioasisiwa na CCM kupitia viongozi hao kuwa ni pamoja na amani na utulivu uliopo hadi sasa, maendeleo ya kijamii na kiuchumi yalioletwa hadi sasa, masuala ambayo yanastahili kuendelezwa na wala si kubezwa. 

Tamasha hilo linajumuisha wasanii kama Odama, Davina, Wastara Juma, Keisha, Wellu Sengo (Matilda), Bi. Mwenda, Mama Lolaa, Mama Nyamayao, Herieth Chumila, Thea, Maya, Chuchu Hans, Steve Nyerere pamoja na wasanii wengine wengi. Aidha alisema kupitia tamasha hilo wasanii hao pamoja na wenzao watazunguka katika mikoa zaidi ya 10 kwa pamoja kufanya kampeni kumnadi mgombea wa urais kupitia CCM, Dk. John Pombe Magufuli, mgombea Mwenza, Samia Hassan Suluhu pamoja na viongozi wengine ngazi mbalimbali wanazogombea kupitia chama cha Mapinduzi. 

 Madhumuni ya tamasha la Mama Ongea na Mwanao 2015 ni kulinda mazuri yote yalioasisiwa na CCM kupitia viongozi wake akiwemo Baba wa Taifa Mwalimu Julias Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume ambayo bila amani mama awezi kujifungua salama, Bila mama hakuna familia, amani inapotoweka mama hawezi kukimbia kilometa kadhaa na kuiacha familia yake, bila mama hakuna ujasiliamali, mama ni kimbilio la baba, kaka, dada na watoto...ikumbukwe kuwa mama ndio mpiga kura ndio maana tunasema mama ongea na mwanao," alisema Wema Sepetu.

 "Na leo hii kuanzia sasa tunatambulisha kampeni yetu tunayoifanya kuhamasisha vijana, kinamama, kinababa, mashabiki wetu wale wote wenye sifa za kupiga kura wapige kura kwa kumchagua kiongozi bora anayetoka Chama Cha Mapinduzi...chagua Dk. Magufuli, Samia Suluhu, wabunge na madiwani wa Chama Cha Mapinduzi," alisema Sepetu. Aidha wasanii hao wamempongeza Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kwa kuongoza vizuri vikao vyote vya chama hicho hadi kupatikana kwa mgombea bora wa urais kupitia chama hicho (Dk. Magufuli), hivyo kuwataka wanaCCM wote ambao waligombea na hawakupata nafasi kuungana na kukitumikia chama. 

"...Mimi Wema Abraham Sepetu nikiwa na baadhi ya wasanii wenzangu ambao tuligombea tunasema muda bado tunao na siku tunazo kwa kukitumikia chama tukipewa ridhaa kwa njia yoyote na kwa nafasi yoyote ndio maana hatuja teteleka tupo imara kuwatumikia wananchi katika nafasi nyingine ndani ya CCM," alisema Sepetu. Imeandaliwa na www.thehabari.com

9 comments:

kidoo said...

Wema na wenzio hamna jipya

Anonymous said...

Pole Wema! na kundi lako kumbuka watu siku hizi wana upeo mkubwa sana! Bla bla kwisha! Sidhani watu wajinga kiasi hicho!

Anonymous said...

Kuleni pesa za zao
Hata wamlete Rihanna , madonna, na mastaa dunia Kura zetu mzee Lowassa na ukawa

Anonymous said...

Kama kawaida Yao CCM hasa kwa wabupumbavu
Waliokosa kura za kutumiwa kwenye kampeni
Mnafikiri mtapata ukuu wa wilaya
Huyo mmoja aliyepita anatosha
Mitaani tu purukushani
Mkiwa bungeni itakuwaje au wakuu wa wilaya
Ukawa ukawa
2015 ikulu yetu

Anonymous said...

Mama ongea na mwanaye
Naomba nisizaliwe na mama hao
Wanawake wa Tanzania kaani mkao wa kula kundi hili hatari
Mtaniambia mimba baada ya uchaguzi

Anonymous said...

Kabisa bila amani usingekuwepo ukawa wala upawa wasanii mmeonyesha tofauti kubwa ya upeo wenu wa akili pamoja na uzalendo wa hali ya juu. Nendeni kawaelimisheni wananchi juu ya upotashaji wa hali ya juu kuhusu mengi mambo mazuri yaliofanywa na CCM. CCM ni taasisi imara barani Africa na duniani kwa ujumla isipokuwa baadhi ya watendaji wake ndio waloiopotoka kwa kujihusisha na ubinafsi baada ya kuweka mbele maslahi ya Taifa kwanza. Lakini la kushangaza zaidi hao wanaojifanya wanataka kuwaletea mabadiliko watanzania wamewachukuwa na kuwafanya kuwa viongozi wa mabadiliko watu wale wale waliojaa mikasfa ya hali ya juu. Taasisi makini haiwezi kumuajiri mtu mwenye kashfa wa ubadhirifu wa mali ya uma ya nchi yake na kuwa ndie chaguo lao la kuwa kiongozi wa nchi hivyo ni vichekesho. Na kila mwenye ndoto ya kwamba ukawa itashinda uchaguzi lazima atakuwa na mtindio wa akili.

Anonymous said...

UKAWA ni genge la wahuni na watu wengine wasiokuwa waadilifu!

Anonymous said...

Oops kampeni toka watu hawa
Mmekwisha ccm
Mnafikiri tunawapenda hawa wala kwetu in kiburudisho baada ya kazi
Watu wasio na maadili yoyote wanaigiza na wanayatenda kikweli loo mungu apishe mbali

Anonymous said...

Hilo mwanamme mmoja
Kulikoni
Toba waume zetu ccm