Friday, January 8, 2016

DK SHEIN AZINDUA TAA ZA KUONGOZEA NDEGE KIWANJA CHA NDEGE PEMBA

PE1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya viwanja vya Ngege Zanzibar Kepten Saidi Iddi Ndumbugani, kuhusu aina ya Taa mbali mbali zilizofungwa kwa uongozaji wa Ndege wakati wa ikitua katika sherehe ya uzinduzi wa Taa za kuongozea Ndege kwenye kiwanja cha ndege cha Pemba uliofanyika jana ikiwa ni katika maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
PE3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya viwanja vya Ngege Zanzibar Kepten Saidi Iddi Ndumbugani, wakati alipofika kutembelea kuona aina ya Taa mbali mbali zilizofungwa kwa uongozaji wa Ndege wakati wa ikitua katika sherehe ya uzinduzi wa Taa za kuongozea Ndege kwenye kiwanja cha ndege cha Pemba uliofanyika jana ikiwa ni katika maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

PE4
Aina ya Taa zilizokuwa mwishoni mwa kiwanja cha ndege cha Karume Pemba zikiwa na Rangi ya Nyekundu na Buluu ambazo hutoa ishara kwa Kepteni anayeongoza Ndege ikitua,Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pamoja na Viongozi mbali mbali aliofuatana nao walijionea taa hizo namna zilivyofungwa katika utaratibu maalum wakati uzinduzi wa Taa za kuongozea Ndege kwenye kiwanja cha ndege cha Pemba uliofanyika jana ikiwa ni katika maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
PE6
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifungua pazia kama ishara ya Uzinduzi wa Taa za Kuongozea Ndege katika kiwanja cha Ndege cha Karume Pemba jana ikiwa ni katika sherehe za shamra shamra za maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (kushoto) Naibu Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Issa Haji Ussi(GAVU).
PE7
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya viwanja vya Ngege Zanzibar Kepten Saidi Iddi Ndumbugani, kuhusu majenereta yanayotoa umeme baada ya kuzindua rasmi Taa za kuongozea Ndege kwenye kiwanja cha ndege cha Pemba jana ikiwa ni katika maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
PE8
Wafanyakazi Mamlaka ya Viwanja vya Ndege na Wananchi wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi wakati alipokuwa akitoa hutuba yake ya uzinduzi wa Taa za kuongozea Ndege kwenye kiwanja cha ndege cha Pemba jana ikiwa ni katika maadhimisho ya miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
PE10
Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Dk. Juma Malik Akili alipokuwa akitoa maelezo ya kitaalam kuhusu mradi wa uwekaji wa Taa za kuongozea Ndege katika sherehe za uzinduzi wa Taa za Kuongozea Ndege katika kiwanja cha ndege cha Pemba jana ikiwa ni katika shamrashamra za miaka 52 ya Mapinduzi Zanzibar.
PE11
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na wananchi katika sherehe za uzinduzi wa Taa za Kuongozea Ndege katika kiwanja cha ndege cha Pemba jana ikiwa ni katika shamra shamra za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,(kulia) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mwanajuma Majid na (kushoto) Naibu Waziri waWizara ya Miundombinu na Mawasiliano Issa Haji Ussi(GAVU).

1 comment:

Anonymous said...

Yaani hizo taa 3 ndie apelekwe Raisi akazindue!!!!!.