ANGALIA LIVE NEWS

Friday, January 23, 2026

WATUHUMIWA WA KUSAFIRISHA KILO 20.03 ZA SKANKA KATIKA BASI LA KING MASAI TOURS WASOMEWA MASHTAKA

WATUHUMIWA wawili, Amasha Iddi Mrisho (40), mkazi wa Buza, Dar es Salaam na Seleman Juma Ally (32), raia wa Msumbiji,  Januari 22, 2026, wamefikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke kujibu tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya skanka.

Akisoma maelezo ya awali ya shtaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mhe. Lukosi, Mwendesha Mashtaka wa Serikali Wakili Nicas Kihembe akisaidiana na Erick alidai kuwa washtakiwa hao walikamatwa tarehe 08 Desemba 2025 katika mtaa wa Wailes, Temeke, Dar es Salaam na maofisa wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya.

Ilidaiwa mahakamani hapo  kuwa, wakati wa operesheni hiyo, DCEA ilikamata pakiti 20 za Bangi aina ya  skanka zenye uzito wa jumla wa kilogramu 20.03, ambazo zilikuwa zimefichwa ndani ya balo la mitumba, kisha kufichwa katika basi aina ya Scania la kampuni ya King Masai Tours, lenye namba za usajili wa Msumbiji AAM 297 CA.

Ilielezwa zaidi kuwa, mashtaka yanayowakabili washtakiwa ni kosa la jinai chini ya kifungu cha 16(I) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, inayokataza umiliki, usafirishaji na biashara ya dawa za kulevya nchini.

Upande wa mashtaka uliieleza mahakama kuwa, shtaka hilo halina dhamana kutokana na uzito wa dawa za kulevya walizokutwa nazo washtakiwa.


Aidha, kwa mujibu wa wakili wa Serikali, upelelezi wa shauri hilo  namba 1535/2026 ya mwaka 2026 bado unaendelea na mashahidi wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hapo siku itakayopangwa.

Shauri hili  lilihairishwa  hadi tarehe 05 februari 2026, huku washtakiwa wakirejeshwa rumande.

Mwisho

Saturday, January 10, 2026

TANI 9 ZA DAWA ZA KULEVYA ZAKAMATWA NCHINI TANZANIA

TANI 9 ZA DAWA ZA KULEVYA ZAKAMATWA NCHINI TANZANIA, BASI LA KING MASAI LANASWA

*Raia wa Kenya akamatwa akitumia biashara ya chai kuficha uuzaji wa dawa za kulevya.
*Basi la King Masai linaswa likisafirisha skanka.
*Mirungi iliyofungwa kama majani ya mwarobaini yakamatwa.
*Watumishi wa serikali wanaswa wakihusishwa na usafirishaji wa dawa za kulevya.

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini imetekeleza operesheni maalum mwishoni mwa mwezi Desemba 2025 na kufanikiwa kukamata jumla ya kilogramu 9,689.833 za dawa za kulevya, sawa na tani 9. Pia pikipiki 11 na magari matatu yamekamatwa, huku watuhumiwa 66 wakitiwa mbaroni kwa tuhuma za kuhusika na biashara hiyo haramu.

Katika operesheni iliyofanyika Sinza C, mtaa wa Bustani, nyumba namba 16 jijini Dar es Salaam, Jefferson Kilonzo Mwende mwenye umri wa miaka 35, raia wa Kenya, alikamatwa akiwa na gramu 131.88 za heroin. Uchunguzi umebaini kuwa mtuhumiwa huyo, ambaye aliishi Tanzania tangu mwaka 2023, alikuwa akitumia biashara ya kuuza chai kama kificho cha kuendesha mtandao wa uuzaji wa dawa za kulevya.

Katika eneo la Wailes, Temeke jijini Dar es Salaam, mamlaka ilikamata pakiti 20 za skanka zenye uzito wa kilo 20.03, zilizokuwa zimefichwa ndani ya balo la nguo za mitumba na kusafirishwa kwa basi aina ya Scania la kampuni ya King Masai Tours, lenye namba za usajili AAM 297 CA kutoka Msumbiji. Basi hilo hufanya safari kati ya Nampula nchini Msumbiji na Tanzania. Watuhumiwa waliokamatwa ni Amasha Iddi Mrisho mkazi wa Buza, Dar es Salaam, pamoja na Seleman Juma Ally, raia wa Msumbiji.

Katika Kinyerezi, mtaa wa Majoka wilayani Ilala, watuhumiwa watatu Erick Ernest Ndagwa, Paul Blass Henry na Tido Emmanuel Mkude walikamatwa wakiwa wanasafirisha bangi yenye uzito wa kilo 193.66 kutoka Morogoro kwenda Dar es Salaam.

Kadhalika, kupitia ukaguzi uliofanyika katika kampuni za usafirishaji wa mizigo jijini Dar es Salaam, paketi 20 za mirungi zenye uzito wa kilo 9.54 zilikamatwa zikiwa zimefungwa na kufanana na majani ya mwarobaini yaliyokaushwa. Mizigo hiyo ilikuwa ikisafirishwa kutoka Kenya kuelekea Australia.

Katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Morogoro, Tanga, Lindi, Kilimanjaro, Njombe, Kigoma na Arusha, operesheni mbalimbali zilifanikiwa kukamata heroin gramu 37.34, skanka kilo 1.015, bangi kilo 7,969.98 na mirungi kilo 1,363.701. Pia mashamba ya bangi yenye ukubwa wa ekari 14 yaliteketezwa.

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imesisitiza wananchi kutoa taarifa pale wanapoona viashiria vya biashara ya dawa za kulevya na kuepuka kubeba mizigo wasiyoijua. Mamlaka itaendelea na operesheni nchi nzima na kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika wote wa uhalifu huu.

Monday, November 10, 2025

GLORY ASHEREHEKEA BIRTHDAY YAKE NA MARAFIKI ZAKE, DURHAM, NORTH CAROLINA

 Birthday girl Glory akifurahia Sherehe ya siku ya kuzaliwa wake aliyesherehekea na ndugu, Jamaa na marafiki zake iliyofanyika siku ya Jumamosi Novemba 8, 2025 Durham, North Carolina.
Dj Luke akimlisha keki mama mwenye Nyumba wake Katika kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake,
Birthday Girl alimlisha keki mums wake Dj Luke Katika kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake 
Birthday Girl akimlisha keki Allena Katika kusherehekea siku Yake ya kuzaliwa siku ya Jumamosi Novemba 9, 2025 Durham, North Carolina.
Kwa Picha zaidi boya soma zaidi

Saturday, October 4, 2025

MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA YATEKETEZA KILO 4,402 ZA DAWA ZA KULEVYA JIJINI DAR ES SALAAM


Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanikisha zoezi kubwa la kuteketeza dawa za kulevya zenye uzito wa jumla ya kilo 4,402.02. Zoezi hilo limefanyika Oktoba 3, 2025, katika kiwanda cha saruji cha Twiga kilichopo Wazo, jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa taarifa ya DCEA iliyosomwa na Kamishna Jenerali Aretas Lyimo, dawa zilizoteketezwa ni pamoja na kilo 2,168.18 za methamphetamine, kilo 1,064.29 za heroin, gramu 326.95 za cocaine, kilo 515.48 za bangi na kilo 653.74 za mirungi. Zote zilikuwa sehemu ya vielelezo vya mashauri mbalimbali yaliyopo mahakamani; baadhi yakiwa tayari yametolewa hukumu na mengine yakiendelea kusikilizwa.


Miongoni mwa mashauri yanayohusiana na dawa zilizoteketezwa ni kesi ya Najim Abdallah Mohamed iliyohusisha heroin kilogramu 882.71 na methamphetamine kilogramu 2,167.29. Aidha, mashauri yaliyotolewa hukumu ni Pamoja na ya Hassan Azizi aliyepatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha, Salum Shaaban Mpangula aliyehukumiwa kifungo cha maisha, Hemed Juma Mrisho maarufu kwa jina la “Hororo” aliyehukumiwa kifungo cha maisha, Ramadhan Shaban Gumbo aliyehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, Irene Dickson Mseluka aliyehukumiwa miaka mitano jela na Gema Victor Mmasy aliyehukumiwa miaka mitatu jela.


Akizungumza wakati wa tukio hilo, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, alisema mamlaka itaendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha vita dhidi ya dawa za kulevya inafanikiwa. Aidha, alisisitiza kuwa DCEA haitabaki katika hatua za kisheria pekee, bali pia itatoa nafasi kwa wale wanaojihusisha na biashara hiyo kuachana nayo kwa hiari.

“Tunatoa msamaha kwa wauzaji wa dawa za kulevya watakaoamua kukiri na kuacha. Hatutachukua hatua yoyote dhidi yao, bali tutashirikiana nao ili kufichua mbinu zinazotumika kuficha na kusambaza dawa hizi,” alisema Lyimo.


Kutokomeza zaidi ya tani nne za dawa za kulevya ni hatua kubwa katika kupunguza athari zinazotokana na biashara haramu ya dawa za kulevya nchini. Tukio hili linadhihirisha dhamira ya DCEA kuhakikisha jamii inalindwa dhidi ya madhara ya dawa hizo ambazo zimekuwa zikiathiri afya, uchumi na usalama wa taifa.



Saturday, August 23, 2025

ONA JINSI TANI 18 4 YA SHEHENA YA DAWA MPYA YA KULEVYA NA WATUHUMIWA WALIVYOKAMATWA


TANI 18.4 YA SHEHENA YA DAWA MPYA YA KULEVYA YAKAMATWA DAR ES SALAAM

Dar es salaam Agosti 13, 2025

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata shehena ya dawa mpya ya kulevya aina ya mitragyna speciosa mifuko 756 yenye uzito wa jumla ya kilogramu 18,485.6 sawa na tani 18.5 iliyokuwa ikiingizwa nchini
kama mbolea.  Hayo yamesemwa leo Agosti 13,2025 na Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kamishna Jenerali Lyimo amesema kuwa, katika tukio hilo watuhumiwa saba (7) wamekamatwa, wakiwemo raia wawili wa nchi ya Sri - Lanka ambao ni Jagath Prasanna Madduma Wellalage (46) na Santhush Ruminda Hewage (25). 

Aliendelea kuwa, watanzania waliokamatwa ni Riziki Abdallah Shawej (40), Andrew Athanas Nyembe (34), Mariam Shaban Mgatila (40), Ramadhan Sanze Said (57) na Godwin Melchory Maffikiri (40).

"Dawa hizi zilikuwa kwenye kontena lenye ukubwa wa futi 40, zikitokea nchini Sri -lanka. 

Hii ni mara ya pili kukamatwa kwa aina hii ya dawa mpya ya kulevya, ambapo mwezi Juni mwaka huu, tulikamata mifuko 450 yenye zaidi ya uzito wa tani 11.5 za dawa hiyo mpya ya kulevya aina ya mitragyna speciosa iliyoingizwa nchini kama mbolea ikiwa kwenye kontena lenye ukubwa wa futi 20 ikitokea nchini Sri - Lanka
ikiwahusisha watajwa hapo juu. 

Hivyo, kufanya jumla ya kilogramu 30,082.03 sawa na tani 30 za dawa hizo kukamatwa kwa kipindi kifupi hapa nchini."

Kamishna Jenerali Lyimo amesema kuwa, Mitragyna Speciosa ni dawa mpya ya kulevya (New psychtropic Substance-NPS) inayotokana na mmea unaofahamika kwa jina la Kratom ambao hupatikana zaidi katika nchi za Kusini Mashariki mwa Bara la
Asia. 

Amesema,dawa hiyo ya kulevya ina madhara sawa na dawa za kulevya jamii ya Afyuni (Heroin, Morphine).

"Dawa hii huathiri mfumo wa fahamu pamoja na kusababisha uraibu na vifo vya ghafla.

Kutokana na kuongezeka matumizi ya dawa ya Mitragym Speciosa duniani, pamoja
na madhara yanayosababishwa na sumu zilizomo katika dawa hii, nchi nyingi duniani zimezuia uzalishaji, usafirishaji na matumizi yake."

Vilevile, Kamishna Jenerali Lyimo amesema kuwa, ukamataji wa Mitragyna Speciosa ni ishara ya kuwepo kwa changamoto mpya katika vita dhidi ya dawa za kulevya nchini. 

Hivyo tutaendelea kuimarisha ufuatiliaji na udhibiti zaidi wa biashara ya dawa hii pamoja na dawa nyingine za kulevya hapa nchini.

Kwa mujibu wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025-2050, jamii yenye afya ni ile ambayo watu wanapata ustawi wa kimwili, kiakili na kijamii ili kujenga taifa la watu wenye uwezo watu wenye uwezo ni nguzo muhimu ya kufikia malengo ya Dira 2050.

Kwa muktadha huo, Kamishna Jenerali Lyimo amesema, matumizi na biashara ya dawa za kulevya yana madhara yakiwemo ya kiafya, kijamii na jiuchumi.

"Hivyo,vita dhidi ya dawa za kulevya kutabadilisha mtindo wa maisha unaozingatia misingi iliyowekwa na kufikia malengo ya Dira ya Taifa mwaka 2050 kwa ufanisi mkubwa kwa kuhakikisha dawa za kulevya zinatokomezwa nchini na kulinda nguvu kazi ya Taifa.

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, inaendelea na kasi ya operesheni katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo kuendelea kuvunja mitandao ya dawa za kulevya na kubaini mbinu mpya za biashara na matumizi ya dawa za
kulevya ikiwemo kuongeza wigo wa utoaji elimu juu ya madhara ya dawa za kulevya kwa lengo la kujenga jamii imara na kulinda ustawi wa jamii kwa maendeleo endelevu,"amesisitiza Kamishna Jenerali Lyimo.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali

MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA
DAWA ZA KULEVYA

SERIKALI YAREJESHA TABASAMU KWA CHIDI BENZ


SERIKALI YAREJESHA TABASAMU KWA CHID BENZ:  AWAASA WASANI KUKAA MBALI NA DAWA ZA KULEVYA
 
SERIKALI ya Awamu ya Sita kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanikiwa kumtibu bure rapa wa muziki wa hip hop nchini, Rashidi Abdallah Mohamed Makwiro (Chid Benz) ambaye kwa miaka kadhaa alitumbukia kwenye uraibu wa dawa za kulevya, hivyo kudhoofika kiafya na kushindwa kutekeleza majukumu yake.

Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo amesema,Chid Benz ni miongoni mwa Watanzania milioni moja ambao wamepatiwa matibabu bure kutokana na uraibu wa dawa za kulevya kote nchini. Ameyasema hayo leo Agosti 22,2025 katika ofisi za DCEA jijini Dar es Salaam wakati akimkabidhi Chid Benz kwa familia na Watanzania baada ya Serikali kumpatia matibabu yaliyodumu ndani ya mwaka mmoja.

Ameeleza kuwa, DCEA licha ya majukumu iliyokasimiwa na Serikali ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya nchini, pia imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kunakuwa na ustawi bora wa jamii nchini. 
"Lakini, jukumu letu lingine ni kuhakikisha kwamba tunajenga ustawi wa jamii ili wale ambao wamekwishajingiza katika matumizi ya dawa za kulevya tunahakikisha kwamba, tunawaondoa kwenye hayo matumizi ya dawa za kulevya."

Amesema kuwa, mafanikio hayo ya kumpatia Chid Benz na watu wengine matibabu yanatokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ikiwemo miundombinu kwa mamlaka hiyo ili kuhakikisha wale ambao wameathiriwa na dawa za kulevya hususani vijana wanawapatia matibabu nchini. Serikali inafanya jitihada hizo kwa kutambua kuwa, vijana ni nguvu kazi ya Taifa, hivyo inapaswa kulinda na kusimamiwa kikamilifu ili ilete matokeo chanya katika uchumi na tija kwa Taifa. Pia, amesema Serikali ina jukumu la kuhakikisha inatibu watu kupitia vituo vya Mat Clinics na kupitia nyumba za upataji nafuu ili kuhakikisha ustawi wa jamii unaendelea kuimarika nchini
"Ni ili kuhakikisha ustawi wa jamii unaendelea kuimarika na nchi inasonga mbele, na isiyokuwa na watumiaji wa dawa za kulevya. Chid Benz alijikuta ameingia kwenye matumizi  ya dawa za kulevya, lakini baada ya DCEA kufanya operesheni kali ambazo zimesababisha dawa za kulevya kuadimika nchini, aliamua kuanza kutumia dawa tiba zenye asili ya kulevya kama mbadala.

Aidha, Kamishna Jenerali amesema, kutokana na Chid Benz kutokuwa na uelewa kuhusu athari za dawa tiba hizo ambazo zinatumika kwa uangalizi maalum kutibu saratani na kufanyiwa upasuaji, zilimuathiri zaidi kiafya. Kutokana na madhara hayo, Serikali ilimchukua Chid Benz na kumpeleka katika kituo cha upataji nafuu cha Pili Missana Foundation kilichopo jijini Dar es Salaam na sasa amepona.

Ameongeza kuwa, kati watu hao milioni ambao kwa nyakati tofauti wamepatiwa matibabu bure na Serikali kote nchini wengi wao ni vijana.
"Tunamtoa Chid Benz kama mfano wa vijana ambao wamepatiwa tiba na Serikali na wanerudi katika hali yao ya kawaida, kwa wanaomzoea Chid Benz kabla ya kupata matibabu na kuchukuliwa na Serikali hali yake ilikuwa mbaya sana na walimzushia kifo."

Amesema, baada ya Serikali kumpatia matibabu sasa afya yake imeimarika na yupo tayari kuanza kuwahudumia wananchi kwa burudani kama zamani na kuhakikisha nchi inaendelea kufurahi kwa kuwa na mwanamuziki hodari.
Chid Benz 

Kwa upande wake, Chid Benz ameishukuru DCEA kwa kumuonesha moyo wa upendo, kwani awali alikata tamaa baada ya kuathiriwa na matumizi ya heroin na dawa tiba zenye asili ya kulevya, lakini sasa yupo imara.
"Kwa kawaida watu husema bahati haiji mara mbili, sasa hivi nipo sawa na karibuni nitarudi mtaani kuendelea na kazi zangu, ninaombeni ushirikiano wenu, ninaishukuru sana mamlaka, ninamshukuru Brother Lyimo (Kamishna Jenerali Lyimo) kwa kunisaidia, Dkt.Mapana nipo bega kwa bega nao na nitafanya kazi kwa bidii."

Aidha, Chid Benz ametoa angalizo kwa wasanii wenzake kuepuka matumizi ya dawa za kulevya kwani si tu kwamba zinaathiri afya, bali pia zinaua ndoto na kipaji.
Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Dkt.Kedmon Mapana ameishukuru DCEA kwa kazi kubwa iliyofanya kuhakikisha msanii Chid Benz anarejea katika hali yake.
Amesema, wakati baraza hilo likimkabidhi Chid Benz kwa mamlaka ili Serikali ikampatie matibabu hali yake ilikuwa mbaya zaidi, lakini leo ana afya njema na anatarajia kuanza kutekeleza majukumu yake ya kimuziki hivi karibuni.

Wakati huo huo, Mkurugenzi wa Pili Missana Foundation, Bi.Pili Missana amewataka Watanzania kuondoa hofu kuhusu muonekano mpya wa Chid Benz.
Amesema, afya ya msanii huyo imeimarika na kuonekana mnene kutokana na matumizi sahihi ya lishe,na si makemikali ambayo alikuwa akiyatumia awali.

#KaziNaUtuTunasongaMbele
#KataaDawaZaKulevyaTimiza

Thursday, August 7, 2025

TAUS CHOIR CONCERT DMV

Unakaribishwa kwenye TAUS CHOIR CONCERT

Wakali wa hizi kazi Zabron Singers kutoka Tanzania kwa kushirikiana na DMV Advent chorale na wengine wengi.

Hili TAMASHA si la kukosa ni Aug 30, 2025 kuanzia 6pm (12 jioni)

Tamasha litafanyikia
Southern Asian Seventh-Day Adventist Church
WAPI
2001 E. Randolph Rd,
Silver Spring, MD, 20904
Milango itakua wazi kuanzia 5:30 pm (11:30) jioni

KIINGILIO
Wakubwa $40
Watoto miaka 13-17 $20
Watoto miaka 5-12 hakuna kiingilio
Lipia tiketi yako kupitia Zelle Bank of America
978 660 3647 jina TAUS INC.
Karibuni

DKT. MWAISOBWA AKABIDHIWA PRESSCARD

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Dkt. Cosmas Mwaisobwa, Msaidizi wa Makamu wa Rais (Hotuba) akipokea Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Presscard) kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) Wakili Patrick Kipangula.

Dkt. Mwaisobwa amepokea Kitambulisho hicho tarehe 05 Agosti, 2025 katika Ofisi za Bodi zilizopo Mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam, baada ya kukidhi vigezo vinavyohitajika Kisheria akiwa na Elimu ya juu iliyotajwa katika Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 ya Daktari wa Falsafa ya Mawasiliano kwa Umma.

Mwaisobwa ni miongoni mwa Wataalamu wachache nchini wenye Elimu ya Udaktari wa Falsafa ya Mawasiliano kwa Umma na Uandishi wa Habari waliopewa vitambulisho, akitanguliwa na Dkt. Egbert Mkoko (Mjumbe wa Bodi) na Dkt. Ayoub Chacha Rioba (Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania TBC).

Akizungumza mara baada ya kumkabidhi kitambulisho hicho, Wakili Kipangula amempongeza Dkt. Mwaisobwa kwa kutekeleza takwa la Kisheria na kuwasihi waandishi wengine ambao bado hawajajisajili kuhakikisha wanafanya hivyo ili waweze kuendelea kutekeleza majukumu yako ya kihabari bila kukinzana na Sheria.

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB imepokea maombi zaidi ya 3,200 kwa ajili ya Ithibati na Vitambulisho vya Uandishi wa Habari na tayari maombi 2,109 yameidhinishwa hadi kufikia tarehe 5 Agosti, 2025 huku maombi 43 kati ya hayo yakikataliwa kutokana na kutokidhi vigezo na 674 yakiwa katika mchakato wa kuthibitishwa.

Tuesday, July 29, 2025

MHE. JESCA MSAMBATAVANGU ASHUKURU KAMATI KUU CCM KUREJESHA JINA LAKE UBUNGE URINGA MJINI


Aliyekuwa mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Mhe. Jesca Msambatavangu ameshukuru kamati kuu kurudisha jina lake katika kuelekea kura za maoni zinazotarajiwa kuanza hivi karibuni kwa siku nne watanadi sera zao kwa Wajumbe wa chama hicho.


Sunday, June 29, 2025

OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA IMEFANIKIWA SANA USHIRIKI WAKE KATIKA KESI ZA DAWA ZA KULEVYA


Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ni mhimili muhimu katika mapambano dhidi ya uhalifu wa dawa za kulevya nchini Tanzania. Katika hatua za awali za uchunguzi wa mashauri ya dawa za kulevya, Ofisi hii hushirikiana kwa karibu na vyombo vya upelelezi pamoja na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ili kuhakikisha ushahidi unakusanywa ipasavyo kabla ya kufikishwa mahakamani. Lengo ni kuhakikisha haki inatendeka kwa misingi ya ushahidi wa kisayansi na kisheria.

Katika kuhakikisha ufanisi wa mashauri haya, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa mashauri yote ya dawa za kulevya yanakamilika kwa hukumu ndani ya kipindi kisichozidi miezi sita. 

Tangu Julai 2024 hadi Juni 2025, jumla ya mashauri 2,785 ya dawa za kulevya yalipelekwa mahakamani ambapo Jamhuri ilishinda mashauri 2,021, sawa na asilimia 63%. Katika kipindi hicho hicho, mafanikio ya jumla ya mashitaka yote ya jinai yaliyosimamiwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ma kusinda yalifikia asilimia 72%. 

Hii ni dalili ya utendaji mahiri na juhudi zinazostahili pongezi katika kulinda usalama wa jamii dhidi ya janga la dawa za kulevya.

Kauli mbiu: "Wekeza kwenye Kinga na Tiba dhidi ya dawa za kulevya"

#DCEA
#OktobaTunatiki

ALLENA AKAMATA NONDO NORTHEN HIGH SCHOOL, DURHAM, NORTH CAROLINA

Picha juu na chini ni Allena akipata Kodak moment mara baada ya kuhitimu high school Darasa la 2025 katika shule ya Northen High iliyopo Durham, jimbo la North Carolina
Allena akikabidhiwanondo Yake ya kuhitimu high school siku ya maafali ya shale hiyo Alhamisi ya June 12, 2025 Katika Ukumbi wa wa chuo kikuu cha Duke.
Wahitimu wa kidato cha 6 akiwemo Allena wakisubili kuitwa kuchukua nondo zao.
Baadhi ya nudge, Jamaa na marafiki waliofika kushuhudia mafaali hiyo ikifanyika.
Mshereheshaji Anna Simtaji akisherehesha situ ya pati kusherehekea kuhitimu kwa Allena high school
Kati ni Allena na mama Yake wakiingia ukumbini.
Mama baba na Mtoto wakifurahia kwa Allena kumaliza high school
Baba na Mwana.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA SOMA ZAIDI

Thursday, June 19, 2025

RAIS WA YANGA AKUTANA NA WANACHAMA NA MASHABIKI WA YANGA USA


Wana Yanga na mashabiki wa Wydad Casablanca wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Yanga Eng. Hersi Said ambae pia ni Mwenyekiti wa vilabu Afrika.

Wana Yanga waliosafiri kutoka New York, DC na mwenyeji wa Hadji walienda hotel aliyofikia Rais wa Yanga mji wa Philadelphia jimbo la Pennsylvania baada ya mechi ya Club World Cup kati ya Wydad na Manchester United na Wydad kupoteza mechi hiyo kwa goli 0-2.

Wana Yanga hao walifanya maongezi na Rais wao kuhusiana na msitakabali mzima wa maendeleo ya Club yao.

Tuesday, June 10, 2025

MAKAMU WA RAIS DKT. PHILIP MPANGO AMEFUNGUA MKUTANO MAALUM WA MKONDO WA BAHARI WA PEMBA -UFARANSA



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati akifungua Mkutano wa pembezoni uliyohusu “Kujenga Uchumi wa Buluu Imara katika Mkondo wa Bahari wa Pemba: Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Bahari kwa Maisha Endelevu na Mabadiliko ya Tabianchi” uliyofanyika kando ya Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Bahari unaofanyika Jijini Nice nchini Ufaransa. Tarehe 10 Juni 2025.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Tanzania imedhamiria kuhakikisha usimamizi endelevu wa mkondo wa Pemba pamoja na ikolojia ya baharini kwa ujumla.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Mkutano wa pembezoni uliyohusu “Kujenga Uchumi wa Buluu Imara katika Mkondo wa Bahari wa Pemba: Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Bahari kwa Maisha Endelevu na Mabadiliko ya Tabianchi” uliyofanyika kando ya Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Bahari unaofanyika Jijini Nice nchini Ufaransa.

Amesema dhamira ya nchi ni kuhakikisha Uchumi wa Buluu unakuwa kielelezo cha ukuaji jumuishi, utunzaji wa mazingira na ustahimilivu wa muda mrefu. Amesisitiza umuhimu wa kufanya kazi pamoja katika kuchukua hatua za haraka ili kulinda Bahari kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Makamu wa Rais amesema Tanzania inachukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na hatari zinazoikumba ikolojia ya Bahari ili kuhakikisha mkondo wa Pemba unakua himilivu pamoja na uendelevu wa mazingira kwa muda mrefu.

WAZIRI MKUU BUNGENI LEO JUNI 10, 2025


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wanafunzi na walimu wa shule ya msingi na awali ya Bahabena iliyopo Kibaha mkoani Pwani katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, Juni 10, 2025 .
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi na walimu wa shule ya msingi na awali ya Bahabena iliyopo Kibaha mkoani Pwani, katika viwanja vya bunge jijini Dodoma, Juni 10, 2025
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Monday, June 9, 2025

SERIKALI IMEENDELEA KUCHUKUA KUKABILI ATHARI ZA MAZINGIRA



Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis wakati akijibu maswali bungeni jijini Dodoma leo tarehe 9 Juni 2025.

Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto za athari za mabadiliko ya tabianchi zinazochangia kuongezeka kwa kina cha bahari na kuathiri fukwe mbalimbali.

Hayo yamesemwa na Naibu wa Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis wakati akijibu swali la Mbunge wa Kilwa Kusini Mhe. Ally Kassinge aliyeuliza Serikali ina mpango gani wa kujenga ukuta eneo la Pwani ya Mji wa Kilwa Kivinje ili kuzuia maji ya Bahari yanayoathiri wananchi.

Mhe. Khamis ametaja hatua hizo kuwa ni pamoja na kuendelea kufanya tathmini ya uharibifu wa fukwe zote katika ukanda wa pwani, kuendelea kutenga na kutafuta fedha kupitia Mifuko ya Usimamizi wa Mazingira na Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi ikiwemo, Mfuko wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi (Adaptation Fund), GEF na GCF na Washirika wa Maendeleo ikiwemo Benki ya Dunia.

Kwa muktadha huo Naibu Waziri Khamis alisisitiza kuwa shughuli za ujenzi wa ukuta katika eneo hilo la pwani zitaanza kutekelezwa baada ya fedha kupatikana.

WAZIRI MKUU: SERIKALI YATENGA 43BN/- KUIMARISHA MICHEZO SHULENI


 * Azindua mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA Iringa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza kwenye uzinduzi wa Mashindano ya UMITASHUMTA na UMISETA kwa Mwaka 2025, ambayo yatafanyika Kitaifa Mkoani Iringa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imetenga sh. bilioni 43 ili kuimarisha michezo katika shule mbalimbali nchini na kati ya hizo, sh. bilioni 32 ni kwa ajili ya kuimarisha Chuo cha Michezo Malya.

Amesema shilingi bilioni 11 zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza mpango wa kuboresha miundombinu ya michezo katika shule za sekondari 10 ambazo ni miongoni mwa shule teule 56 za michezo nchini.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatatu, Juni 9, 2025) wakati akifungua mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi na Sekondari Tanzania (UMITASHUMTA na UMISSETA) kwenye viwanja vya Kichangani vilivyoko Kihesa, mkoani Iringa.

Akielezea mikakati ya Serikali ya kuendeleza michezo na sanaa nchini, Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejipanga kuimarisha Chuo cha Michezo Malya ili kiendelee kutoa mafunzo kwa kuzingatia utaalam na kuimarisha ufundishaji wa masomo ya michezo shuleni.

Sunday, June 8, 2025

RAIS WA ZANZIBAR DK.HUSSEIN ALI MWINYI ALIHUTUBIA BARAZA LA EID AL ADHAA UKUMBI WA DKT.ALI MOHAMED SHEIN SUZA TUNGUU MKOA WA KUSINI UNGUJA


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasili katika viwanja vya Ukumbi wa Dkt.Ali Mohamed Shein SUZA Tunguu kwa ajili ya kulihutubia Baraza la Eid Al-Adha lililofanyika katika ukumbi huo, baada ya kumalizika kwa Sala ya Eid Al-Adha, na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Alhajj Dkt.Haroun Ali Suleiman
GWARIDE Maalumu la Kikosi cha FFU lililoandaliwa kwa ajili ya Baraza la Eid Al-Adha wakitowa heshima kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi, lililofanyika katika viwanja vya Ukumbi wa Dkt.Ali Mohamed Shein SUZA Tungui Mkoa wa Kusini Unguja leo 7-6-2025

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akipokea salamu ya heshima kutoka kwa Kikao cha FFU, wakati wa Gwaride maalumu lililoandaliwa kwa ajili ya Baraza la Eid Al-Adha, lililofanyika katika viwanja vya ukumbi wa Dkt.Ali Mohamed Shein SUZA Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja leo 7-6-2025.

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA FEDHA MWANDUMBYA ATETA NA UJUMBE WA KAMPUNI YA ALSTOM


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bw. Elijah Mwandumbya, akiongoza kikao na ujumbe wa Kampuni ya ALSTOM, ambapo pamoja na mambo mengine walijadiliana kuhusu uendelezaji wa miundombinu jijini Dar es Salaam, kikao hicho kilifanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini, Dodoma.
Mkurugenzi wa Miradi na Fedha, Ofisi ya ALSTOM, Bi. Julie Morel, akifanya wasilisho kuhusu utekelezaji wa mradi wa miundombinu jijini Dar es Salaam wakati wa kikao na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini, Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya ALSTOM, nchini Tanzania, inayojihusisha na uwekezaji katika ujenzi na uendeshaji wa miundombinu ya reli duniani, Bi. Kefilwe Mothupi, baada ya kumalizika kwa kikao kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.

SIO JAMBO JEMA WAZAZI KUWALAZA WATOTO WENYE JUNSIA TOFAUTI CHUMBA KIMOJA


Na Issa Mwadangala.
Wazazi na Walezi Mkoani Songwe wametakiwa kutowachanganya watoto wenye jinsi tofauti katika chumba kimoja ikiwa ni pamoja na kuwalaza chumba kimoja na ndugu, jamaa au marafiki wanaowatembelea ili kuepuka vitendo vya ukatili ikiwa ni pamoja na mahusiano ya kimapenzi.

Kauli hiyo ilitolewa Juni 08, 2025 na Afisa Mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Akama Shaaban wakati akitoa elimu ya madhara ya ukatili wa kijinsia kwa wazazi/walezi na watoto waliofika kucheza michezo mbalimbali katika Kituo cha kutambua na kukuza vipaji vya watoto kiitwacho Mwakitwange Toto Center kilichopo maeneo ya Isangu Wilaya ya Mbozi ili kujionea mambo wanayoshiriki watoto hao kituoni hapo.

"Tafiti mbalimbali zimeonesha kuwa vitendo vya watoto kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi vinaanzia majumbani ambapo watoto wenye jinsi mbili tofauti wanalala chumba kimoja ikiwa ni pamoja na wageni wanaowatembelea na wakati mwingine hata kitanda kimoja, jambo hilo hupelekea kuanza mahusiano wakiwa wadogo na kuhatarisha mfumo wao wa akili. Pia imebainika kuwa kuchanganya au kuchukua badaboda tofauti tofauti kunapelekea watoto kufanyiwa ukatili pindi waendapo na watokapo shuleni, hivyo niwaombe wazazi mlio hapa kutokufanya hivyo tafuteni bodaboda mmoja mnaemuamini na kumjua vizuri ili endapo mtoto atafanyiwa ukatili iwe rahisi kumbaini mhusika" alisema ACP Akama.

Thursday, June 5, 2025

MADAKTARI BINGWA WAMTIBU MZEE ALIYEKUWA NA TATIZO LA KUOZA SEHEMU YA UTUMBO.


Na John Walter -Manyara
Madaktari Bingwa wa Rais Samia wamefanikiwa kumfanyia upasuaji wa utumbo mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka (69) ambaye jina limehifadhiwa aliyeteseka na tatizo hilo kwa zaidi ya miazi sita.

Hali hiyo imebainika Juni 04, 2025 ambapo mwananchi huyo alifika Hospitalini hapo akiwa na maumivu makali na kushindwa kufanya shughuli za maendeleo.

Kwa mujibu wa Madaktari Bingwa hao walibaini sehemu ya utumbo mpana ikiwa imejikunja kwa nyuzi 720, hali iliyosababisha utumbo huo kujaa na kuharibika na kuonyesha dalili za utumbo kuoza.

"Aliletwa jana hapa tukamfanyia vipimo na tukabaini utumbo mpana ulikuwa umejifunga, tukamuandaa kwa ajili ya upasuaji, wakati wa upasuaji tumekuta utumbo umejikunja zaidi ya mara mbili, umejaa na kuoza ikabidi tukate sehemu ya utumbo uliooza na hadi sasa mgonjwa anaendelea vizuri" amesema Dkt Julius Mollel, Daktari Bingwa wa usauaji.

Tuesday, June 3, 2025

TUINUKE PAMOJA – MIDAHALO YA KIJAMII KUELEKEA USAWA WA KIJINSIA


Na John Walter -Dodoma

Katika jitihada za kujenga jamii yenye usawa na haki kwa wote, mradi wa Tuinuke Pamoja unaotekelezwa na TGNP kwa kushirikiana na Aga Khan Foundation na kufadhiliwa na Ubalozi wa Ireland, umeendelea kuleta mwamko na majadiliano ya kina kupitia midahalo ya kijamii inayofanyika katika kata za Kidoka (Chemba), Keikei na Suruke (Kondoa).

Midahalo hii inalenga kuchambua kwa kina vikwazo vinavyozuia upatikanaji wa usawa wa kijinsia katika jamii na kutafuta suluhu endelevu kwa changamoto zinazojitokeza. Kwa kuzingatia umuhimu wa ushirikishwaji, midahalo inawahusisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kijamii na wa dini, wazee wa mila, wazee maarufu, vikundi vya kijamii pamoja na watu wenye ulemavu.

Katika midahalo hiyo, washiriki wamekuwa wakieleza uzoefu wao kuhusu masuala ya kijinsia, mila na desturi zinazokwamisha maendeleo ya wanawake na wasichana, pamoja na mapendekezo ya jinsi jamii inaweza kuondokana na mifumo kandamizi. Kupitia mchakato huu shirikishi, jamii inahimizwa kufikiria upya mitazamo na mienendo inayozuia maendeleo jumuishi.