Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
nchini (TFF), Jamal Malinzi amemshukuru Rais wa CECAFA, Leodgar Tenga
kwa kuipa Tanzania uenyeji wa mashindano ya Vilabu Bingwa Afrika
Mashariki na Kati (Kagame Cup) iliyomalizika jana kwa klabu ya Azam
FC kutawazwa Mabingwa wapya wa michuano hiyo.
Aidha Malinzi ameishukuru Kamati ya
Ndani ya Uendeshaji ya Michuano hiyo (LOC) kwa kazi nzuri
waliyoifanya ya kuandaa na kuhakikisha michuano hiyo inafanyika na
kumalizika katika hali ya usalama na amani.
Malinzi pia amewapongeza wapenzi,
washabiki na wadau wa soka nchini waliojitokeza kushuhudia michezo ya
michuano hiyo na kuonyesha nidhamu ya hali ya juu ndani nan je ya
uwanja kipindi chote cha michuano.
Rais Malinzi ameipongeza klabu ya
Azam FC kwa kutwaa Ubingwa Kagame, kwa kutwaa ubingwa huo imeweza
kuweka historia ya kutwaa Ubingwa huo kwa mara ya kwanza tangu
kuanzishwa kwake na pia kuwa klabu iliyocheza michuano hiyo na kuwa
Bingwa bila kuruhusu nyavu zake kutikisika.
Pia Malinzi amewashukuru waandishi
wa habari/vyombo vya habari kwa sapoti yao wakati wa michuano hiyo.
Shukrani hizo pia zimepelekwa kwa klabu za Yanga SC, KMKM kwa
kushiriki mashindano hayo.
U-15 YAREJEA KUTOKA ZANZIBAR
Kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana
wenye umri chini ya miaka 15 (U-15), kimerejea leo asubuhi kutokea
kisiwani Zanzibar kilipokwenda kucheza michezo ya kujipima nguvu na
kombani ya U-15 ya kisiwani humo.
Katika michezo miwili iliyocheza
kisiwani humo, iliweza kushinda michezo yote miwili, (4-0 ), (1-0),
huku kocha Bakari Shime akiwapongeza vijana wake na kusema
wanaendelea kuimarika kuelekea kujiandaa na kuwania kufuzu kwa
fianali za Mataifa Afrika chini ya miaka 17 mwakani.
Baada ya kurejea jijini Dar es
salaam leo, kambi ya timu hiyo imevunjwa na vijana hao watakutana
tena mwisho wa mwezi wa Agosti kama ilivyo katika program yao ya
kukutana kila mwisho wa mwezi na kucheza michezo ya kirafiki.
Mwishoni mwa mwezi Agosti timu hiyo
ya vijana inatarajiwa kuelekea mkoani Tanga kucheza michezo ya
kirafiki na kombani ya mkoani humo, ambapo kocha wake Shime pia
anatumia nafasi hiyo kutazama wachezaji wengine wenye uwezo mzuri
katika timu za kombaini za mikoa kwa ajli ya kuwaongeza katika kikosi
chake.
Mpaka sasa timu hiyo ya vijana chini
ya miaka 15 (U15) imeshafanya ziara na kucheza michezo katika miji ya
Mbeya na kisiwani Zanzibar.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA
MIGUU TANZANIA (TFF)
No comments:
Post a Comment