Advertisements

Saturday, June 18, 2016

POLISI YAWAONDOA WAMACHINGA WALIOKAIDI AMRI YA KUWATAKA KUONDOKA MTAA KONGO

 Askari Polisi wakizima moto uliokuwa umewashwa na wafanyabiashara ndongondogo ‘maarufu kwa jina la wamacchinga’ waliokuwa wamepanga bidhaa zao chini katika katika mtaa wa Kongo jijini Dar es Salaam leo, wakipinga kuondolewa katika mtaa huo. (Picha na Francis Dande)
 Polisi wakizima moto uliowashwa na wamachinga.
 Askari wakiwa wameimarisha ulinzi katika mtaa wa Kongo.
 Zoezi la kuzima moto likiendelea.
 Mtaa wa Kongo ukiwa mweupe baada ya kuondolewa kwa wamachinga.
 Wanachi wakipita katika Mtaa wa Kongo bila usumbufu wowote baada ya wafanyabiashara wanaopanga bidhaa zao chini kuondolewa na Polisi leo.
 Gari la Polisi likiwa katika mtaa wa Kongo. 
 Polisi wakiwa Diria.
 Garoi la Polisi likimwaga maji kuzima moto uliokuwa unawaka. 
 Wananchi wakipita kandokando ya magari ya Polisi.
 Polisi wakizima moto.
Mtaa wa Kongo ukiwa mweupe baada ya Polisi kuondoa wamachinga waliokuwa wamepanga bidhaa zao chini.

6 comments:

Anonymous said...

Huu ni utawala wa kidikteta kila mahali kuanzia wananchi wa kawaida wafanyakazi na viongozi wanaushutumu huu utawala wa magufuli

Anonymous said...

Ninaingia wasix2 na uelewa wako wa neno dikteta.
Anyway, huu ni utawala unaosimamia sheria na natambua itachukua muda kwa watu wa namna yako kuchange mindset zenu. Yale maisha ya ujanjax2 hayana nafasi tena.

Anonymous said...

Wewe anonymous wa saa 1:40 pm June 2016, usiwe mjinga hivyo utawala wa Mtukufu Rais Magufuli ni utawala wa sheria!! Simple & Clear! Sasa sijui mnataka nini watu Kama wewe Kama kiongozi wa kupigania nchi na wananchi wake amepatikana na anafanya kazi yake na inaonekana mnaanza kumtuhumu ni Dictator that's Non sense!

Anonymous said...

Mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi. Law enforcement means dictatorship?

Anicetus said...


Mazingara ya kufanya biashara ni lazima yawe safi ili kuzuia magonjwa, usafi wa mji na maendeleo biashara pamoja na ulipaji kodi za mapato. Wakati wa awanu ya Nyererre wamachinga walipewa sehemu zao kufanya biashara na hakukuwa na matatizo yeyote. Kwa mfano, hapa New york-USA, wamachinga wote wamepewa sehamu zao za kufanya biashara. Anayesema serikali ya Magufuli ni ya kidikteta anatakiwa atembee miji mingine duniani aone jinsi miji ziko safi na wafanya biashara wanaongeza maendeleo ya nchi zao. Keep Dar es Salaam Clean.

Mr. Ally said...

Siyo udikteta ila watu hawaheshimu sheria.Kitu ambacho serikali inaweza kufanya ni kupanga siku za weekends ziwe market day. Wafunge mtaa mmoja na kila mtu alete vitu vyake kuuuza. Lakini lazima watozwe ushuru na City oli hela hizo zifanye kazi ya kusafisha mazingira.