Thursday, August 20, 2015

ZANZIBAR MWENYEJI WA MKUTANO WA MAONESHO YA ZAO LA KAHAWA KWA MARA YA KWANZA MWAKANI 2016

Viongozi wa Wizara ya Biashara Zanzibar wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakimsubiri Mgeni Rasmin kumpokea wakiwa katika viwanja vya Hoteli ya Serena Shangani Zabnzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe Abdallah Mwinyi Khamis alipowasili katika viwanja vya Hoteli ya Serena Shangani Zanzibar kwa ajili ya Uzinduzi wa Mkutano wa Maonesho ya Kahawa unaotarajiwa kufanyika mwakati Febuari 2016, utafanyika kwa mara ya kwanza Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Coffee Board Eng Adolph A Kumburu, alipowasali katika viwanja vya hoteli ya Serena Zanzibar. kwa ajili ya ufunguzi wa mkutano huo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Meneja Mkuu wa BADERSH, Ndg. Abdallah Bagersh, kutoka Ethiopia Mwenyekiti wa Bodi ya Umoja huo. alipowasali katika viwanja vya hoteli ya Serena Zanzibar. kwa ajili ya ufunguzi wa mkutano huo

Makamu wa Pili wa Rais wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiongozana na Naibu Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Zanzibar Mhe Thuwaiba Kisasa kuelekea ukumbi wa Mkutano huo uliofanyika hoteli ya Serena Shangani Zanzibar.
Balozi Seif akizungumza na Viongozi wa Mkutano huo kabla ya kuaza mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Serena Shangani Zanzibar.
Muongozaji wa Mkutano huo akitowa maelezo ya madhumuni ya mkutano huo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na kuwatambulisha kabla ya kuaza kwa mkutano. huo uliofanyika hoteli ya Serena Zanzibar.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Coffee Board Eng Adolph A Kumburu, akizungumza wakati wa mkutano huo kutowa maelezo machache kwa washiriki.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wakulima wa Kahawa (AFCA) kutoka Ethiopia ,Ndg Abdallah Bagersh, akizungumza wakati wa uzinduzi wake kuhusiana na Zao la Kahawa, unaotarajiwa kufanyika Zanzibar kwa mara ya kwanza mwakani na kuwashirikisha wakulima wa kahawa na maonesho ya kahawa mbalimbali wakati wa mkutano huo.
Naibu Waziri wa Biashara Masoko na Viwanda Zanzibar Mhe Thuwaiba Kisasa akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kuufungua Mkutano wa maandalizi ya Maonesho ya Kahawa unaotarajiwa kufanyika Zanzibar kwa mara ya kwanza Zanzibar.mwakani mwezi wa Feb 2016
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiufungua mkutano wa maandalizi ya Mkutano wa Maonesho ya Kahawa katika ukumbi wa hoteli ya Serena Zanzibar, Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Zanzibar kwa mara ya kwanza na kuhudhuriwa na wakulima wa Kahawa na Wafanyabiashara wa zao hilo
Wajumbe wa Mkutano huo wakimsikiliza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akiwahutubia katika ukumbi wa hoteli ya Serena Shangani Zanzibar.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia hutuba ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif
Picha zote kwa hisani ya ZanziNews

No comments: